Waziri
wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), (kulia),
akipongezwa na baadhi ya Mawaziri, baada ya kuwasilisha Mapendekezo ya
Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2022/23 na Mfumo na
Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23, wakati wa Mkutano wa
Wabunge wote.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- WFM).
Waziri
wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiwasilisha
Mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka
2022/23 na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23,
katika Mkutano wa Wabunge wote jijini Dodoma, ambapo Serikali imepanga
kutumia shilingi trilioni 41.06.
Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) (kulia)
akifurahia jambo wakati wa Mkutano wa Wabunge wote jijini Dodoma ambapo
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb),
akiwasilisha Mapendekezo ya Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka
2022/23 na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba (kushoto)
pamoja na baadhi ya viongozi wa Wizara hiyo, wakifuatilia uwasilishaji
wa Mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka
2022/23 na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23,
katika Mkutano wa Wabunge wote jijini Dodoma.
Baadhi
wa viongozi wa Idara wa Wizara ya Fedha, Watumishi wa Bunge na Wabunge
wakifuatilia uwasilishaji wa Mapendekezo ya Serikali ya Mpango wa
Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2022/23 na Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya
Serikali kwa mwaka 2022/23, katika Mkutano wa Wabunge wote jijini
Dodoma.
Baadhi
wa viongozi wa Idara wa Wizara ya Fedha, wakiwa katika Ukumbi wa Pius
Msekwa, jijini Dodoma wakisubiri kuwasilishwa kwa Mapendekezo ya
Serikali ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2022/23 na Mfumo na
Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2022/23, wakati wa Mkutano wa
Wabunge wote.
No comments:
Post a Comment