SERIKALI
ya Tanzania ni miongoni mwa nchi 130 zilizoweza kushiriki katika
Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo na Mazingira ambayo huwa yanafanyika
kila mwaka na kwa mwaka huu yanafanyika kuanzia tarehe 10 hadi 14 Machi,
2022 katika jiji la Doha nchini Qatar.
Aidha,
maonesho haya yamejumuisha kampuni za Kimataifa 300, wakulima 100
pamoja na wawasilisha mada wapatao 56 kutoka mataifa mbalimbali.
Maonesho
yalifunguliwa Machi 10, 2022 na Waziri wa Wizara ya Manispaa na
Mazingira ( Ministry of Municipality and Environment), Mhe. Abdulla bin
Abdulaziz bin Turki Al Subaiel.
Lengo kuu la maonesho haya ni kutoa fursa kwa washiriki kuonesha bidhaa na huduma zinazohusiana na kilimo na mazingira.
Meneja
Kanda ya Ziwa Victoria, Bw.Jarome Kayombo wakibadilishana uzoefu wa
teknolojia ya uhifadhi wa taka zitokanazo na mabaki ya chakula ( food
waste) kwenda kutengeneza mbolea. Ameahidi kushirikiana na NEMC kwa
kuleta teknolojia hiyo mbadala nchini Tanzania.
Pia
maonesho haya yanawapa fursa washiriki kubadilishana uzoefu,
technologia pamoja kutafuta masoko na fursa na uwekezaji katika kilimo
na usimamizi wa mazingira.
Baraza la Taifa la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ni miongoni mwa taasisi 19 zilizoshiriki kutoka Tanzania.
Tanzania
tulikuwa na jumla ya mabanda 19 ambapo kati yake 17 ni kutoka taasisi
za Serikali zinazoshughulika na Mazingira, Kilimo, Ufugaji na Uwekezaji.Mhandisi
Jane Kadoda ambaye ni Afisa Mazingira Mwandamizi akitoa elimu juu ya
huduma mbalimbali zinazotolewa na NEMC kwenye maonesho Kimataifa ya
Kilimo na Mazingira nchini Qatar.
Baadhi
ya taasisi za Serikali ni pamoja na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania
-Qatar, NEMC, TIC, Bodi ya Korosho, Bodi ya Maziwa, Bodi ya Chai, Bodi
ya Kahawa, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanyangiko pamoja na Umoja wa
Kilimo cha Mbogamboga.
Washiriki
wengine kutoka Tanzania ni pamoja na MamboJambo Design, Dumas African,
Greencom African Ltd, Natural Shine Traders na Kampuni ya Oasisi Import
Export Ltd.
Baraza
la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira liliwakilishwa na Meneja
wa Mawasiliano na Uhusiano wa Umma, Bi. Irene John, Meneja wa Kanda ya
Ziwa, Bw. Jarome Kayombo pamoja na Mhandisi Jane Kadoda kutoka Kanda ya
Morogoro Rufiji.Washiriki
kutoka NEMC wakijadili baadhi ya maoni na mapendekezo yaliyotolewa na
washiriki mbalimbali waliotembea banda la NEMC nchini Qatar.
Miongoni
mwa wageni waliotembelea banda la NEMC siku ya ufunguzi ni pamoja na
Balozi wa Tanzania nchini Qatar, Mhe. Balozi Mahadhi Juma, Balozi wa
Burundi – Qatar, taasisi za Serikali, Wizara na Kampuni mbalimbali
kutoka nchi washiriki kama vile Wizara ya Manispaa na Mazingira, Kitengo
cha Hifadhi ya Bahari wakiwakilishwa na Prof. John Man Kon Wong,
Kampuni ya CITC wanaojihusisha na ufungaji mitambo ya kupunguza hewa
ukaa kwenye magari, teknolojia ya kuongeza tija kwenye kilimo na
mazingira.
Kampuni
ya Royal Link hawa wanajihusisha na Uzalishaji na Usambazaji wa
Chemikali za Viwandani, Kampuni za kusafisha maji taka na maji ya
Bahari.
Aidha,
mwananchi mmoja mmoja kutoka Qatar na nchi mbalimbali walitembelea
banda la NEMC ili kupata elimu pamoja ma kuelezwa fursa za uwekezaji
kwenye mazingira, utalii na kilimo.
Akizungumza
katika maonesho hayo , Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Bi.
Irene John amesema, maonesho hayo yatafungua fursa nyingi za uwekezaji
katika bidhaa na huduma kwani kupitia mawasilisho yaliyofanywa siku ya
ufunguzi tarehe 10 Machi, 2022 NEMC imeonesha jinsi gani mazingira ya
uwekezaji yameboreshwa kupitia mifumo mbalimbali ya kielektroniki kama
vile mchakato wa utoaji vibali vya Tathimini ya Athari kwa Mazingira (
TAM) na pia mfumo wa upatikanaji wa vibali vya taka hatarishi ambao uko
katika hatua za mwisho kukamilika.
Kupitia
Meneja wa Kanda ya Ziwa, Bw. Jarome Kayombo amebainisha kuwa moja ya
faida kubwa kwa NEMC kushiriki katika maonesho ya Kimataifa ya Mazingira
na Kilimo ni pamoja na kuitangaza NEMC na pia kutoa elimu juu ya
utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa uwekezaji endelevu.
Aidha,
maonesho yametoa fursa ya fursa za uwekezaji na kuelemisha washiriki
juu ya mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira Nchini Tanzania.
Pia
maonesho haya yametoa fursa ya kubadilishana uzoefu wa technologia
mbadala za kutunza mazingira zitakazoleta tija katika kuboresha maisha
ya kila siku.
No comments:
Post a Comment