Mkuu wa Mkoa wa Arusha John
Mongella amezindua maonyesho ya kimataifa ya kilimo TANZFOOD EXPO huku
zaidi ya makampuni 120 kutoka Tanzania na nchi jirani zikishiriki
Maonesho
hayo yameandaliwa na kampuni ya KILIFAIR Promotion na kuzinduliwa jana
tarehe 11/3/2022 katika viwanja vya magereza vilivyopo jijini Arusha
Baada
ya kutembea mabanda mbalimbali yaliyoshiriki,Mkuu wa Mkoa Arusha John
Mongella alisema maonyesho hayo ni ya siku tatu katika viwanja hivyo na
lengo kubwa ni kuleta tija katika mnyororo mzima wa thamani katika
kilimo,ufugaji,uvuvi pamoja na uchakataji
Mongella alisema kuwa
kupitia maonyesho hayo wadau wa kilimo watapata fursa za elimu katika
kujifunza na biashara huku serikali ya mkoa ikipania kufanya kimataifa
Kwa
upande wake Mkurugenzi mtendaji wa TAHA Dkt,Jackline Mkindi ambaye pia
ni mwenyekiti wa baraza la kilimo Tanzania alisema kwa sasa sekta ya
kilimo imefunguka na ndio inashikilia uchumi wa Taifa
"Masoko yamefunguka sana bidhaa za Tanzania zinagombaniwa kwenye masoko ya kimataifa "alisema Dkt Mkindi
Pia
aliongeza kuwa Tanzania ni nchi yenye fursa ya kilimo ukizingatia
imezungukwa na nchi nyingi barani Afrika ambazo zinahitaji bidhaa kutoka
Tanzania
"Uwepo wa taarifa muhimu za wazalishaji ziliwezesha
TAHA kushiriki katika mikutano mikubwa ya kimataifa kama Dubai,Ufaransa
pamoja na ubelgiji kuangalia fursa za masoko"alisema Dkt Mkindi
Mkurugenzi
wa KILIFAIR Promotion,Dominic Shoo alisema kuwa maonyesho hayo ni fursa
kwa wananchi kuweza kujifunza mbinu mbalimbali za kufanya biashara
pamoja na kubadilishana mawazo na fursa zilizopo
Mkuu wa Mkoa Arusha John Mongella akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kuzindua maonesho ya kimataifa ya TANZFOOD
No comments:
Post a Comment