KATIKA
kuadhimisha kilele cha Siku ya Ustawi wa Jamii Duniani yenye kauli mbiu
“Juhudi jumuishi dhidi ya ukatili wa aina zote kwa maendeleo endelevu”
Taasisi ya Ustawi wa Jamii ikishirikiana na Chama cha watoa huduma za
Ustawi wa Jamii Tanzania (TASWO) na Umoja wa Mashirika yasiyo ya
Kiserikali ya Ulinzi na Huduma za Ustawi wa Jamii (TaCosWe) na wadau
wengine watatoa huduma za ustawi wa jamii bure kwa wananchi wote siku ya
kilele cha maadhimisho ya siku ya Ustawi wa Jamii Duniani Machi 15,2022
na kuendelea.
Akiongea
katika mkutano na waandishi wa habari Mkuu wa Taasisi ya Ustawi wa
Jamii, Dkt.Joyce Nyoni,amesema ni mwaka wa 15 sasa wanaadhimisha Siku ya
Ustawi Duniani kote tangu ilipoanza kuadhimishwa mwaka 2007.
Amesema,
ili kuiishi kauli mbiu ya mwaka huu taasisi na wadau watatoa huduma ya
ushauri wa masuala ya ndoa na mahusiano, masuala ya watoto
waliotelekezwa na ushauri wa kisaikolojia na nyingine nyingi pamoja na
kutoa elimu kwa wananchi kuhusu hasa nini maana ya Ustawi wa Jamii na
wawatumie vipi wataalam hao kutatua changamoto za kila siku kwenye
maisha.
"Nawakaribisha wananchi wote kupata huduma za jamii na elimu zitakazotolewa bure katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii,"amesema.
Naye
Mwenyekiti wa Chama cha Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Tanzania
(TASWO),Dkt. Mariana Makuu amesema, “Sababu kubwa ya ukatili unaoendelea
hapa nchini ni afya ya akili, tunawakaribisha wananchi wote waje
waongee na wataalamu ambao watawasaidia kutatua matatizo yao,”amesema.
Kwa
upande wake Katibu wa Umoja wa mashirika yasio ya kiserikali ya ulinzi
na huduma za jamii,Bi. Hilda Ngaja amesema, "Tunashirikiana na Serikali
na wadau wengine katika kustawisha jamii yetu na kuondoa tatizo hili la
ukatili linaloendelea nchini kwetu,"amesema.
No comments:
Post a Comment