Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani (kushoto) akiongoza
leo na Mkuu wa Wilaya ya Sikonge John Pallimgo (kulia) na viongozi
wengine kwenda kuangalia Banda lililo eneo hatarishi ambalo wachimbaji
wa Madini wa Mgodi wa Kitunda walikuwa wakishinikiza kuwepo Shule.
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani viongozi wengine wakiwa
katika Banda lililo eneo hatarishi ambalo wachimbaji wa Madini wa Mgodi
wa Kitunda walikuwa wakishinikiza kuwepo Shule.
Afisa
Elimu wa Wilaya Sikonge Isack Thomas akisoma taarifa leo kwa Mkuu wa
Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani (kushoto) jinsi Banda lililo
eneo hatarishi ambalo lilijengwa na wachimbaji wa Madini wa Mgodi wa
Kitunda na kutaka kulifanya kuwa Shule.
Mkuu
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani (katikati) akitoa maagizo
leo kwa viongozi wa Wilaya ya Sikonge baada ya kutembelea Kibanda
ambacho kiko katika eneo hatarishi ambacho kilikuwa kikitumiwa na watoto
wa wachimbaji madini wa mgodi wa Kitunda kama shule.
Picha na Tiganya Vincent
***********************************
NA TIGANYA VINCENT
MKUU
wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilida Buriani ameuagiza uongozi wa
Wilaya ya Sikonge kuwaondoa watoto wote ambao wanaishi katika eneo la
uchimbaji madini la Kitunda na kuwapeleka Kijijini kwa ajili ya usalama
wao.
Alisema lengo ni kuwaondoa katika hatari mbalimbali
zinazoweza kuwakabili kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini na
kuhakikisha wanakwenda kuishi Kijijini ambapo watapata huduma za elimu.
Balozi Dkt. Batilida ametoa kauli hiyo baada ya kutembelea eneo hilo
kwa ajili ya kujionea Kibanda ambacho kianzishwa na wachimbaji wa madini
na baadhi ya watendaji wamekuwa wakishinikiza kuanzishwa kwa shule ya
Msingi.
“Watoto wote na mama zao waliomo kwenye Mgodi wanatakiwa
kuondoka na kwenda Kijijini …humu mgodini watabaki wanaume…ni makosa
watoto kuendelea kuishi humo…tukiwakuta tena tutalizimika kusitisha
shughuli za uchimbaji ,jambo ambalo hatuki litoke” alisisitiza.
Mkuu
huyo wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilida aliagizwa kubomolewa kwa
Kibanda kilichojengwa katika eneo la Mgodi kwa kutaka kukigeuza Shule ya
Msingi.
Alisema Kibanda hicho kilipojengwa ni hatari kwa watoto
kwa kuwa kipo karibu eneo la kuchanganyia kemikali kwa ajili ya
kuchenjulia dhahabu na pembeni yake kuna shimo lenye maji yenye kemikali
hatari zinatumika kusafishia dhahabu ambazo ni hatari kwa maisha ya
bianadamu.
Balozi Dkt. Batilida aliongeza karibu na Kibanda
hicho upo mchanga ambao una mabaki ya kemikali ambazo zimetumika
kuchenjuliwa dhahabu na hivyo kuhatarisha maisha ya watoto kama
wakiushika.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alisema Serikali
inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inatoa shilingi milioni 900
kila mwezi kwa ajili ya bure kwa Mkoa wa Tabora.
Balozi Dkt.
Batilida alisema kufuatia hali hakuna haja ya kuwa na kibanda hicho kwa
kuwa Shule ambayo ni rasmi ya Misheni ipo katika Kijiji cha Kitunda nayo
inapata fedha kwa ajili ya elimu bure.
Katika hatua nyingine
Balozi Dkt. Batilida ameuagiza uongozi wa Wakala wa Huduma wa Mistu
Tanzania(TFS) kukagua maeneo yote ili kujiridhisha kuwa hakuna wananchi
wanaishi ndani yake na kuendesha shughuli kinyume cha Sheria za
Uhifadhi na nyingine za Nchi.
Alisema sanjari hilo ameiagiza
Ofisi ya Madini kupitia migodi yote ya Mkoa wa Tabora ili kuhakikisha
hakuna vitendo ambavyo vinavunja Sheria za Nchi vinafanyika katika
maeneo hayo ikiwemo vya ujenzi wa vibanda kwa ajili ya shule zisizo
rasmi.
Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu alisema
Watumishi ambao walishindwa kusimamia taratibu na kuachangia wananchi
wajenge Kibanda hicho kinyume cha Sheria mbalimbali katika eneo hilo
watachukuliwa hatua.
Alisema taratibu za uanzishaji Shule
zinajulikana na zipaswa kufutwa pindi wananchi wanataka kuanzisha Shule
katika eneo lao.Makungu alisema Mtendaji wa Kata na Afisa Elimu Kata
wameshindwa kusimamia majukumu yao na ndio maana watoto wamejaa katika
eneo la Mgodi wakati walipaswa kuwa katika Shule rasmi.
Kibada hicho kijengwa mwezi uliopita na kuanza kukusanya watoto katika eneo hilo Mwezi huo huo.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Saturday, September 18, 2021
Home
Unlabelled
RC TABORA AAGIZA WATOTO WANAOISHI KATIKA MGODI WA KITUNDA WAONDOLEWE
RC TABORA AAGIZA WATOTO WANAOISHI KATIKA MGODI WA KITUNDA WAONDOLEWE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment