Na Linda Shebby ,Rufiji Mkoani Pwani
BENKI
ya NMB imekabidhi viti na meza 50 vyenye thamani ya Shilingi Mil4.5
kwa Shule ya Sekondari Utete iliyopo Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani.
Akikabidhi
samani hizo Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Mashariki Harold Haule
Lambilaki alisema kuwa meza na viti hivyo vilivyotolewa vimetokana na
faida ambayo Benki ya NMB wanazipata ambapo wamejikita kurejesha kwa
jamii katika miradi ya elimu, afya, ambapo pia hutoa vitanda na
magodoro hasa katika hospital za vijijini na mjanga yanayotokea kwa
dharura.
"Hadi hivi Sasa tayari NMB tumesha toa misaada yenye thamani ya Bili.8" alisema Kaimu Meneja Kanda ya Mashariki Lambileki
Akizungumza
Mara baada ya kupokea samani hizo Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja
Edward Gowelo aliwashukuru NMB kwa kutoa viti na meza kwa Shule hiyo ya
utete huku akiwasisitiza wanafunzi pamoja na uongozi wa Shule hiyo
kutunza ipasavyo samani hizo Ili ziweze kuwafaa wanafunzi wengine
watakao kuja kusoma baada yao.
Naye Kaimu Afisa Elimu Wizara ya Msingi Mwalimu Fatuma Kimolo alitoa Shukran kwa NMB kwa kutoa msaada huo.
Mwalimu
Mkuu wa Shule hiyo ya Utete Bassa Hilary Ngela alisema kuwa shule hiyo
ilianzishwa mwaka 1940 ambapo ilikua Shule ya Msingi na baadaye
ikapandishwa daraja kuwa shule ya Sekondari mwaka 1990 kwa sasa
inawanafunzi 1361 ambapo wavulana 837 na wasichana 524 huku
akibainisha kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa
majengo, bwalo la kulia chakula kwa wanafunzi na upungufu wa vitanda vya
kulalia wanafunzi hivyo amewaomba wadau mbalimbali kuwasaidia kutatua
changamoto hizo.
Mwalimu Ngella alisema kuwa anatoa shukran kwani msaada huo itasaidia kupunguza uhaba viti na madawati shule ni hapo.
No comments:
Post a Comment