A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, September 18, 2021

BENKI YA NMB YATOA VITI NA MEZA VYENYE THAMANI YA MILIONI 4 SEKONDARI YA UTETE, RUFIJI MKOANI PWANI

Na Linda Shebby ,Rufiji Mkoani Pwani

BENKI ya NMB imekabidhi viti na meza 50  vyenye thamani ya Shilingi Mil4.5 kwa Shule ya Sekondari Utete iliyopo Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani.

Akikabidhi samani hizo Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Mashariki Harold Haule Lambilaki alisema kuwa meza na viti hivyo vilivyotolewa  vimetokana na faida  ambayo Benki ya NMB wanazipata ambapo wamejikita kurejesha kwa jamii katika miradi ya  elimu, afya, ambapo pia hutoa vitanda na magodoro hasa  katika  hospital za vijijini na mjanga yanayotokea kwa dharura.

"Hadi hivi Sasa tayari NMB tumesha  toa misaada yenye thamani ya Bili.8" alisema Kaimu Meneja Kanda ya Mashariki Lambileki

Akizungumza Mara baada ya kupokea  samani hizo  Mkuu wa Wilaya ya Rufiji  Meja  Edward Gowelo  aliwashukuru NMB kwa kutoa viti na meza kwa Shule hiyo ya utete huku akiwasisitiza wanafunzi pamoja na uongozi wa Shule hiyo kutunza ipasavyo samani hizo Ili ziweze kuwafaa wanafunzi wengine watakao  kuja kusoma baada yao.

Naye Kaimu Afisa Elimu Wizara ya Msingi Mwalimu Fatuma Kimolo  alitoa Shukran kwa NMB kwa kutoa msaada huo.

Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ya Utete Bassa Hilary Ngela  alisema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1940 ambapo ilikua Shule ya Msingi na baadaye ikapandishwa daraja kuwa shule ya Sekondari mwaka 1990  kwa sasa inawanafunzi 1361 ambapo wavulana 837 na wasichana   524 huku akibainisha kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa majengo, bwalo la kulia chakula kwa wanafunzi na upungufu wa vitanda vya kulalia  wanafunzi hivyo amewaomba wadau mbalimbali kuwasaidia kutatua changamoto hizo.
Mwalimu Ngella alisema kuwa  anatoa shukran kwani msaada huo itasaidia  kupunguza uhaba  viti na madawati shule ni hapo.






 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages