A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, June 24, 2019

Msuva ajifunga KMC FC kwa miaka miwili


Timu ya Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, KMC imefanikiwa kumuongezea mkataba mshambuliaji wake, James Msuva ambapo sasa ataendelea kuwatumikia waajiri wake hao hadi mwaka 2021.

James Msuva ni mdogo wake na mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania na Klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco, Simon Msuva ambaye alijiunga na Waarabu hao Julai 29, mwaka jana kwa dau la dola 150,000, sawa na zaidi ya Sh milioni 337 akitokea Yanga.

“Wakati tukiendelea na maandalizi ya KAGAME CUP leo James Msuva ameongeza mkataba wa miaka miwili na kuendelea kusalia KMC hadi mwaka 2021.“- KMC FC

James Msuva alijiunga na KMC akitokea katika klabu ya Mbao FC ya Mwanza kwa mkataba wa mwaka mmoja mwaka 2018

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages