A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, January 31, 2018

Kenya yamfananisha Odinga kama Alshabaab

Kenya yamfananisha Odinga kama Alshabaab
Serikali ya Kenya kupitia kwa Waziri wa Usalama, Dkt Fred Matiang’i,  imelipiga marufuku kundi la National Resistance Movement (NRM) lililo chini ya Muungano wa Upinzani (NASA) nchini humo na kulitangaza kuwa ni kundi la kihalifu.
Kundi hilo limeundwa baada ya Raila Odinga kususia uchaguzi wa marudio na limekuwa katika harakati za kutaka mabadiliko katika uchaguzi na kuwashawishi wananchi kususia bidhaa za makampuni ambayo yanadiwa kuwa upande wa serikali ya nchi hiyo.

Aidha, waziri huyo ameliweka kundi la NRM kwenye ordha moja na makundi ya kigaidi ya Al Shabaab na Al Qaeda ambapo hatua hii imekuja ikiwa ni baada ya Raila Odinga kujiapisha kama Rais wa Watu wa Kenya.
Ifuatayo ni taarifa ya rasmi ya serikali kulitangaza NRM kuwa kundi la kihalifu:


MAKUNDI MENGINE YALIYOTANGAZWA KUWA NI YA KIHALIFU NCHINI HUMO:
1. Al-Shabaab
2. Amachuma
3. Angola Msumbiji
4. Banyamulenge
5. Baghdad Boys
6. Charo Shutu
7. Chinkororo
8. Coast Housing Land Network
9. Congo by Force
10. Dallas Muslim Youth
11. Forty Brothers
12. Forty-two Brothers
13. Jeshi la Embakasi
14. Jeshi la Mzee
15. Jeshi la King’ole
16. Japo Group
17. Kamjesh
18. Kamukunji Youth Group
19. Kaya Bombo Youth
20. Kenya Youth Alliance
21. Kosovo Boys
22. Kuzacha
23. Makande Army
24. Mombasa Republican Council
25. Mungiki Movement, Mungiki Organisation, Mungiki Sect
28. Republican Revolutionary Council
29. Sabaot Land Defence Force
30. Sakina Youth
31. Sungu Sungu
32. Siafu
33. Taliban

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages