Mbunge
wa jimbo la Kibaha vijijini Amoud Jumaa ambaye alikuwa mgeni rasmi
akizungumza katika mkutano wa uchaguzi mkuu wa Jumuiya ya vijana (UVCCM)
Wilaya ya Kibaha vijijini ambao uliofanyika katika ukumbi wa JKT Ruvu
Mlandazi, ambapo katika uchaguzi huo Juma Mbonde alichaguliwa kuwa
Mwenyekiti mpya kwa kupata kura 230 katika ya kura 253 zilizopigwa.
JUMUIYA
za umoja wa vijana (UVCCM) zimetakiwa kumuunga mkono Rais wa
serikali ya awamu ya tano Dk. John Magufuli katika kuhakikisha wanafanya
kazi kwa bidii na kuwa wazalendo na nchi yao ili kuweza kutimiza
azma ya kuwa na Tanzania yenye uchumi wa viwanda na kuwaasa kuachana
kabisa na masuala ya kuwa tegemezi kila kukicha.
Kauli
hiyo imetolewa na Katibu wa (UVCCM) Mkoa wa Pwani Ramadhani Kapeto
wakati wa mkutano maalumu wa uchaguzi wa jumuiya ya umoja wa vijana
katika Wilaya ya Kibaha vijijini ambao umefanyika katika ukumbi wa JKT
Ruvu mlandizi.
Katibu
huyo alisema kwa sasa vijana hususn wa UVCCM wanatakiwa kubadilika na
kuwa na mtazamo chanya wa kujikita zaidi katika kutafuta fursa zilizopo
za kuanzisha miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itaweza kuwasaidia
kuwapatia kipato ambacho kitaweza kuwasaidia katika kujikimu kimaisha
na kupambanana wimbi la umasikini kuliko kukitegemea chama pekee
kiwasaidie.
“Vijana
hasa wa UVCCM mimi napenda kuwaambia kuwa inabidi kujituma kwa hali na
mali kwa lengo la kuweza kukipogania chama chenu, pamoja na kuhakikisha
mnakuwa na kazi yoyote ambayo inakuingizia kipato na sio kuwa omba omba
hivyo ni vema mkawa na miradi yenu mbali mbali ambayo itakuwa ni
mkombozi mkubwa kuliko kukitegemea chama, kazi za chama ni kujitolea
hakuna ajira hivyo ni vema mkalifahamu hilo,”alisema Katibu huyo.
Kwa
upande wake Mbunge wa jimbo la Kibaha vijijini Amoud Juma amewataka
vijana hao wa UVCCM kuhakikisha wanashikamana kwa hali na mali kwa
lengo la kuweza kushinda katika chaguzi mbali mbali na kuweka mipango
madhubuti katika kukiimarsiha chama cha mapinduzi kiweze kushinda katika
chaguzi za ngazi mbali mbali zinazokuja.
Aidha
Mbunge huyo ambaye pia ni mlezi wa UVCCM Kibaha vijijini alibainisha
kuwa katika kuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuwa na
uchumi wa viwanda atahakikisha anaweka mipango madhubuti na kuandaa
program maalumu ya kuviwezesha vikundi mbali mbali vya vijana kwa
lengo la kuweza kujikwamua na wimbi la umasikini pamoja na kuweza kuleta
mabadiliko chanya ya kimaendeleo.
“Kwa
upande wangu mimi kama wa jimbo hili la Kibaha vijijini lengo langu
kubwa ni kuwasaidia vijana waweze kutimiza malengo yao na kwa sasa nipo
katika mipango ya kuendelea kuwawezesha katika vikundi nia na madhumuni
ni kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na wimbi la
umasikini,”alifafanua Jumaa.
Aidha
Mbunge huyo aliongeza kuwa katika kuunga juhudi za Rais wa awamu ya
tano atahakikisha kwamba anawapatia mafunzo mbali mbali ya ujasiliamari
pamoja na kuwapatia mitaji vijana hao ili waweze kuingia katika kufanya
biashara pamoja na kuwa na viwanda vidogovidogo ambavyo vitaweza
kuwawezesha kujiajiri wao wenyewe.
KATIKA
kinyang’anyoro cha uchaguzi huo wa jumuiya ya umoja wa vijana (UVCCM)
katika Wilaya ya Kibaha vijijini imeweza kupata safu mpya ya uongozi
ambao utaongoza kwa kipindi cha miaka mitano, huku Jumanne Mbonde
akichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya baada ya kupata kura 230 kati ya kura
253 ambazo zilipigwa na wajumbe wa mkutano huo kutoka kata 14.
No comments:
Post a Comment