Kamishna
Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa kwanza kutoka
kushoto akikagua vichochoro vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kuingia
nchini katika kijiji cha Mugulika Kata ya Bwerenyange wilaya ya
Karagwe Mkoani Kagera. Kamishna Jenerali yuko mkoa wa Kagera kujionea
shughuli zinazotekelezwa na Idara yake mkoani humo.
Kamishna
Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa kwanza kutoka
kushoto akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe mkoa
wa Kagera Godfrey Mheluka watatu kutoka kulia katika kijiji cha
Muguluka Kata ya Bwerenyange wilaya ya Karagwe Mkoa wa
Kagera.Kamishna Jenerali huyo amefanya ziara katika Vipenyo
vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kutoka nchini nyingine kuingia
Tanzania.
Kamishna
Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala wa nne kutoka kulia
akiwa katika Mkutano wa Hadhara na baadhi ya Wananchi (hawapo pichani)
wa Kijiji cha Muguluka Kata ya Bwerenyange wilaya ya Karagwe Mkoa wa
Kagera.Kamishna Jenerali huyo amefanya ziara katika Vipenyo
vinavyotumiwa na wahamiaji haramu kutoka nchini nyingine kuingia
Tanzania.
Baadhi
ya Wananchi wa Kijiji cha Muguluka Kata ya Bwerenyange wilaya ya
Karagwe Mkoa wa Kagera wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Idara ya
Uhamiaji Dk. Anna P. Makakala katika Mkutano wa Hadhara baina ya
wanakijiji hao na Ujumbe huo wa Idara ya Uhamiaji kutoka Makao Makuu
ambapo katika Mkutano huo Dk. Makakala alitoa wito kwa wanakijiji
hao kutowahifadhi wahamiaji haramu kwenye makazi yao sambamba na
kuwataka kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola pale wanapogundua kuna
mgeni asiyeeleweka na wanamtilia mashaka kwenye makazi yao.(Picha zote
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
No comments:
Post a Comment