AFISA
Tarafa ya Mihambwe mkoani Mtwara, Emmanuel Shilatu amefanya ziara
kujiridhisha uhalisia wa upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wote wa
shule za msingi na sekondari zilizopo Tarafa ya Mihambwe ambapo
ameridhishwa na upatikanaji huo wa chakula lishe kwa wanafunzi.
Gavana
Shilatu alijionea uhalisia wa wanafunzi wakipewa kifungua kinywa,
chakula cha mchana na chakula cha usiku kwa wa walio hosteli ambapo
alitoa pongezi kwa hatua hiyo kubwa ya uzingatiaji lishe kwa wanafunzi.
"Napenda
niwapongeze wazazi na walimu kwa namna wanavyoendelea na utaratibu wa
kuzingatia suala la lishe kwa wanafunzi. Upatikanaji chakula unaimarisha
elimu na afya kwa mtoto. Ni jukumu la kila mdau wa elimu kuhakikisha
lishe inazingatiwa kwa wanafunzi kutokana na umuhimu wake," amesema
Gavana Shilatu mara baada ya ziara.
Serikali
ilitoa mwongozo kupitia Wizara ya Elimu kuhakikisha wanafunzi wote
wanapatiwa lishe shuleni kwa ajili kuimarisha elimu na afya. Jambo
ambalo linatekelezwa vyema kwa shule zote za msingi na sekondari
zilizopo Tarafa ya Mihambwe.
No comments:
Post a Comment