Na Farida Said, Morogoro.
Jeshi
la polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata raia 17 wa Ethiopia wakiwa
katika gari aina ya Toyota Alphard wakielekea mkoani Mbeya baada ya
dereva wa gari hilo kushindwa kusimama katika kizuizi cha Mikumi mkoani
humo.
Hayo yamelezwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro,
Fortunas Musilimu wakati akizungumza na waandishi wa habari Marchi 5
ambapo amesema jeshi hilo limewakamata raia hao Machi 4, 2022 eneo la
Ruaha Mbuyuni baada ya dereva wa gari hilo kutiliwa shaka na polisi.
Hata
hivyo kamanda huyo amesema pia jeshi hilo limewakamata watuhumiwa 50
kwa tuhuma mbalimbali katika operesheni ya kupambana na uhalifu
iliyoanza Februari 26, 2022.
“Operesheni hii ya kupambana na
uhalifu, ilianza Februari 26 hadi Marchi 4 mwaka huu na tayari
tumewakamata watuhumiwa 46 wakiwemo raia 17 wa Ethiopia na operesheni
hii itakuwa endelevu na kuhakikisha wahalifu wanaacha uhalifu.”amesema
Kamanda Musilimu.
Kamanda amesema katika operesheni hiyo
imewatia nguvuni watuhumiwa 16 wanaojihusisha na kuuza na kusambaza
bhangi ambapo viroba vinne vyenye jumla ya kilo 80 huku vijana 13
wakikamatwa kwa kujihusisha na wizi maeneo ya masoko na katika minada ya
Kikundi, Sabasaba na soko la Mawenzi.
No comments:
Post a Comment