Mradi mkubwa wa upanuzi wa bandari ya Tanga umefikia asilimia 26 wa ujenzi wake huku ukitarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu
Akizungumza
na waandishi wa habari jana katika maonesho ya TANZFOOD,Mhandisi Hamis
kipalo alisema mradi huo upo nyuma ya muda kutokana na changamoto
mbalimbali ikiwemo ya ugonjwa wa Covid 19 iliyosababisha nchi nyingi
kufunga mipaka
"Ugonjwa wa Covid 19 ulisababisha vifaa vya ujenzi
kutoingia nchini kutokana na nchi nyingi kufunga mipaka yao"alisema
Mhandisi Kipalo
Aliongeza kuwa mradi huo ukikamilika utaleta
manufaa makubwa kwa nchi katika kuongeza ufanisi wa bandari kutoka tani
laki saba na nusu hadi tani Milioni 30
"Uwezo wa bandari utaongezeka na pia itasaidia biashara katika ukanda wa kaskazini na Afrika Mashariki "alisema Mhandisi Kipalo
Naye
Afisa uhusiano wa bandari ya Tanga,Adam Shindo alisema ushiriki wao
katika maonyesho hayo ni kusogea karibu na wateja wao nakutumia fursa
hiyo kwa kujitangaza zaidi
"Kilichotuleta hapa ni kusogea karibu
na wateja wetu na kuwaelezea maendeleo ya mradi,upanuzi wa bandari ya
tanga "alisema Shindo
Mradi huo unatekelezwa na kampuni ya CHEC
kutoka China na kusimamiwa na Mhandisi mshauri kutoka Denmark
ikishirikiana na kampuni ya Kitanzania Anova
Afisa uhusiano wa bandari ya Tanga Adam Shindo akizungumza na vyombo vya habari katika maonyesho ya kimataifa TANZFOOD jijini Arusha
Mhandisi Hamisi Kipalo akizungumza na waandishi kuhusu maendeleo ya mradi mkubwa wa upanuzi wa bandari ya Tanga
No comments:
Post a Comment