Spika
Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kamishna wa
Sensa nchini Mhe. Anna Samamba Makinda amekuwa miongoni mwa wageni
walioshiriki usiku wa chakula cha pamoja uliowakutanisha wasanii zaidi
ya 200 wanaotarajia kutumbuiza kwenye Tamasha kubwa dunia la Muziki la
Serengeti linalofanyika jijini Dodoma Machi 12 na 13, 2022.
Dhifa hiyo ya chakula cha jioni imekuwa ya aina yake ambapo wasanii wamepata fursa ya kuelimisha umuhimu wa sensa.
Aidha,
kuelekea kesho kwenye tamasha la Serengeti wasanii mbalimbali
wakiongozwa na Bushoke wamekonga nyoyo za wa wageni mbalimbali
walioshiriki usiku huu.
Mbali
na viongozi Wakuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo,wageni
wengine ni wabunge na wakuu wa taasisi mbalimbali za fedha na binafsi na
watu mashughuli.
Aidha, wasanii wamepata nafasi ya kubadilishana mawazo na viongozi mbalimbali wa makampuni walioshiriki.
Mdhamini Mkuu wa shughuli hii ni CRDB.
Serengeti inakwenda kufanyika kesho ikiwa ni mwaka mmoja toka kuingia madarakani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan
No comments:
Post a Comment