KAMATI
ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo,Mifugo na Maji imeitaka Serikali kuwekeza
nguvu zaidi katika kutoa elimu kwa umma juu ya udhibiti wa sumukuvu ili
kupunguza madhara yanayosababishwa na sumukuvu.
“Tunaipongeza
Serikali kwa ujenzi wa maabara ya udhibiti wa magonjwa ya kibaolojia ya
mimea,ambayo kukamilika kwake kutasaidia sana kupunguza matumizi ya
kemikali kama viuatilifu katika mimea katika kudhibiti magonjwa na
mashambulio ya wadudu waharibifu katika mimea.
"Aidha
serikali ihakikishe inatoa elimu kwa umma na hasa kwa wakulima wadogo
wadogo juu ya udhibiti wa sumukuvu katika mimea na kuelimisha wakulima
juu ya matumizi ya wadudu marafiki katika kudhibiti magonjwa ya
mimea,”amesema Dkt.Ishengoma.
Akitoa
maelezo ya awali Naibu Waziri wa Kilimo,Mhe. Anthony Mavunde
ameishukuru Kamati ya Bunge kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kusimamia na
kuishauri serikali katika masuala yahusuyo kilimo na kuahidi kuyafanyika
kazi maelekezo yaliyotolewa.
>Kujenga maghala 14 ya kuhifadhi mazao ya chakula;
>Ujenzi wa kituo mahiri cha usimamizi wa mazao baada ya kuvuna (Post harvest Center of Excellency)
>Ujenzi wa Maabara Kuu ya Kilimo.
No comments:
Post a Comment