A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, April 30, 2021

SIMBA SC KUIVAA KAIZER CHIEFS YA AFRIKA KUSINI

 

Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara na Wawakilishi wa Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC watacheza na Klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini katika mchezo wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League).

Michezo ya mkondo wa kwanza itachezwa kati ya Mei 14 na 15, 2021 ambapo Simba SC atakuwa ugenini wakati mchezo wa marudino utakaopigwa kati ya Mei 21 na 22 Wekundu wa Msimbazi watakuwa nyumbani, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Endapo Simba SC itapita hatua ya Robo Fainali itacheza na mshindi kati ya MC Algers ya Algeria au Wydad Casablanca ya Morocco kati ya Juni 18 na 19, 2021 na mchezo wa marudiano kati ya Juni 25 na 26, 2021.

Michezo mingine ni Al Ahly SC ya Misri dhidi ya Mamelodi Sundowns, MC Algers ya Algeria dhidi ya Wydad Casablanca na CR Belouzdad ya Algeria dhidi ya ES de Tunis ya Tunisia.

Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho, Pyramids FC ya Misri watacheza na Enyimba FC ya Nigeria, Orlando Pirates ya Afrika Kusini wao watapambana na Raja Casablanca Coton Sports ya Cameroon dhidi ya ASC Jaraaf ya Senegal na CS Sfaxien ya Tunisia dhidi ya JS Kabylie ya Algeria.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages