A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, April 16, 2021

FLAVIANA MATATA FOUNDATION YAGAWA BURE TAULO ZA KIKE 'SANITARY PADS' SHULE YA WASICHANA JANGWANI

 Taasisi ya Flaviana Matata Foundation chini ya Mwanamitindo Flaviana Matata imetoa taulo za kike (Sanitary Pads) kwa Wasichana wenye uhitaji 100 kutoka Shule ya Wasichana ya Jangwani, huu ni mwanzo wa kugawa taulo hizi kwa Wasichana watakaonufaika na Kampeni yao ya 'Donate A Period'. kupitia vituo vya mafuta vya TOTAL.


“Wasichana hawa watapata taulo za kike bure kwa mwaka mzima ambapo kila Msichana atapata “packet” moja na nusu kila mwezi, kipekee kabisa tunawashukuru TOTAL na kila aliyeshiriki kwa kujitoa kwao kuhakikisha tunawafikia Wasichana wengi zaidi kwa kujaza mafuta katika vituo vya TOTAL kwa mwezi March”,alisema Flavina

Alisema kuwa jumla wamepokea kiasi cha Tsh. 18,184,003 ambazo zinasaidia Wasichana 420 kwa mwaka mzima, kila Msichana atapokea paketi 18 kwa mwaka, hivyo inafanya idadi ya Wasichana wanaopokea taulo zetu bure kila mwezi kufikia 1720 kwa ujumla na kati ya hao 300 ni kutokana na asilimia 10 ya faida inayopatikana katika mauzo ya Lavy Sanitary pads. 

“Tunatambua hedhi ni kikwazo kwa wasichana wengi wanao toka kwenye mazingira magumu kote mijini na vijijini kukosa masomo siku 3-5 kila mwezi kwa sababu hawawezi kumudu gharama za taulo za kike, tutawahiza Wadau mbalimbali kuunga jitihada hizi kwa namna moja au nyingine tuhakikishe hedhi siyo kikwazo kwa Mtoto wa Kike kupata elimu”,alieleza Flavi
na.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages