A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, July 15, 2020

MULTICHOICE YAUNGANA NA UN KWENYE KAMPENI MAALUM YA COVID-19

Mwenyekiti Mtendaji wa kundi
la makampuni ya MultiChoice,
Imtiaz Patel.
Julai, 2020: Kundi la makampuni ya MultiChoice limetangaza mkakati wao mpya wa kusaidia katika kupambana na janga la COVID19 kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa (UN) ambapo wamezindua kampeni maalum ya kukabiliana na usambazaji wa taarifa zisizo sahihi kwa umma.

Kampeni hiyo imezinduliwa kwa kuzingatia ukweli kuwa kumekuwa na taarifa zisizo sahihi na ambazo hazitoki katika vyanzo na mamlaka husika na mara nyingi taarifa hizo huleta taharuki, woga na hofu kwa umma na hivyo kuathiri jitihada za kupambana na janga a COVID-19 kote duniani.

Tangu kulipuka kwa ugonjwa huo, MultiChoice imekuwa mstari wa mbele katika kupambana nao ambapo ilianza kutumia vyombo vyake kutoa matangazo ya tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona pamoja na kutoa misaada mbalimbali ya vifaa muhimu vya kukabiliana na ugonjwa huo.

Katika muendelezo huo, sasa MultiChoice imeungana na umoja wa mataifa kwenye kampeni mahsusi ijulikanayo kama ‘Pause’ ambayo inawaasa watu kuacha kutunga au kusambaza habari zisizothibitiswa na mamlaka stahiki kuhusu COVID-19 kwakuwa habari hizo zinaleta madhara kwa umma.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages