A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, July 15, 2020

BENKI YA NMB YASISITIZA UWEZESHAJI NA USHIRIKISHAJI WAZAWA

Mkuu wa Idara ya Huduma za Kifedha kwa Biashara za Kimataifa wa Benki ya NMB, Linda Teggisa, akizungumza wakati mabalozi wa nchi nane (Misri, Pakistani, Uturuki Kenya, Uganda, Falme za Nchi za Kiarabu na Sweden) wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini walipotembelea Banda la Benki ya NMB kwenye maonyesho ya Saba saba.
Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Urusi, Rifat Pateev akizungumza na Ofisa wa Benki ya NMB, BatuIi Sunna wakati mabalozi wa nchi kumi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini walipotembelea Banda la Benki ya NMB kwenye maonyesho ya Saba saba.
Benki ya NMB inaupa uwezeshaji na ushirikishaji wazawa kipaumbele katika kuchangia kwake utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo humu nchini, hasa ile endelevu ya kimkakati iliyoanzishwa na Serikali.

Sera hii ya benki hiyo ambayo pia inatumika kwenye kufadhili uwekezaji, ni mpango wake wa makusudi kusaidia uendelezaji na ushiriki wa Watanzania na biashara zao katika ujenzi wa taifa na maendeleo yake kwa ujumla.

Hiyo ni kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Huduma za Kifedha kwa Biashara za Kimataifa wa Benki hiyo - Bi. Linda Teggisa, aliyetoa ufafanuzi huo baada ya kuupokea ujumbe wa Mabalozi nane walioambatana na uongozi wa Chemba ya Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) walipotembelea banda la Benki ya NMB kwenye Maonyesho ya Saba Saba ambayo yanafungwa rasmi leo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages