A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, June 29, 2019

Halmashauri Kuu Ya Mkoa Wa Arusha CCM Yapokea Utekelezaji Wa Ilani Ya Uchaguzi Ya CCM 2015-2020

Halmashauri Kuu ya mkoa wa Arusha CCM imepokea Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020 Kwa kipindi cha Robo Tatu ya Mwaka wa Fedha Julai-March 2019.

Akizungumza katika ufunguzi wa Kikao hicho Katibu mkuu wa CCM mkoa Mussa Matoroka amesema kuwa kabla ya kufanya kikao hicho walifanya ziara katika wilaya zote zilizopo mkoani humo kukagua shughuli za maendeleo na kujiridhisha.

Mrisho Gambo amesema kuwa hali halisi ya mapato katika mkoa huu ni ndogo ukilinganisha na matumizi kwa mwaka huku akisema kuwa serikali kuu imekuwa ikiibeba mkoa ili kukukidhi mishahara ya wafanyakazi mkoani humu.

Aidha amesema serikali imefanya mambo mengi Sana katika mkoa huu Kama za ujenzi wa barabara  za lami na sisizo za lami huku, kujenga madaraja ya kiwango kizuri ili kurahisha huduma za kijamii pamoja na upatikanaji  wa mkoani maji ya kutoka mkoani hapa.

Aidha amesema kuwa Serikali kwa nguvu kubwa imeweka nguvu kubwa katika kujenga barabara la lami yenye kilimita 49 Wilayani Ngorongoro jambo ambalo halijawahi kufanyika tangu uhuru wa Tanzania bara.

Katika uwasilishaji huu, Mrisho Gambo amesema kuwa Serikali pia imewezesha upatikanaji wa maji ya kutosha kwa asilimia mia moja pindi mradi utakapokamilika na wanachi wote mkoa ni watapata maji safi na salama ukilinganisha na asilimia 40 ya maji
 yanayopatikana kwa sasa.

Kuhusu huduma za afya, Mrisho Gambo amesema ametoa fedha za kujenga hospitali za Wilaya katika zote mkoani Arusha hivyo kufanya Kila wilaya kuwa na hospitali yake huku akisema kuwa bado serikali imejenga vituo vipya vya afya katika mkoa mzima wa Arusha.
 
Aidha  Gambo amewataka viongozi wa dini kuendelea kuiombea na nchi na kudumisha na kuhubiri Amani katika ibada zao kwani ikiondoka hakuna atayeweza kuirejesha Ameongeza kuwa miradi hiyo inayosimimamiwa na kutekelezwa na  Serikali haijapata msaada wowote toka nje, amesema yote ni mapato na makusanyo ya ndani.

Naye kamishna Msaidizi wa Mkoa wa Arusha Jonathan Shani amesema kuwa katika kutekeleza ilani ya CCM, Jeshi la Polisi mkoani hapa wanatekeleza kwa kudumisha ulinzi na Usalama kama jina lijulikanavyo la Geneva of Africa.

Aidha ametoa onyo kali kwa watakaojaribu kuhamasisha ama kujaribu kuandama huku akisema kuwa wanaendelea kuhakikisha Arusha itakuwa mbali na madawa ya kulevya.

Ameongeza kuwa Jeshi la Polisi lipo kuwalinda wananchi wote ila akatoa wito kwa kwa wanawake kuwa ulinzi upo kwao na Kila atakayemtesa mwanamke atachukuliwa hatua stahiki kwa wanaowanyanyasa wake zao.

Hata hivyo kamanda huyo amesema kuwa ulinzi katika mkoa wa Arusha na mipaka yake upo imara na kwamba wananchi wote wasiwe na shaka

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages