A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, May 20, 2019

KWA JAMBO HILI RC MAKONDA MUNGU ANAKUONA.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Mhe. Paul Makonda, akizungumza wakati wa hafla ya kugawa vyakula kwa ma imamu  kutoka katika misikiti zaidi ya 1000
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Mhe. Paul Makonda, akikabidhi chakula kwa mmoja wa maimamu waliofika katika hafla ya kugawa vyakula kwa ma imamu zaidi ya  misikiti1000 wa jiji hilo. Kushoto kwa mkuu wa mkoa  ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa kata ya Vingunguti Omary Kumbilamoto, na wengine ni wawakilishi kutoka ubalozi wa Falme za Kiarabu pamoja na sheikh mkuu wa Dar es Salaam.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ahmad Mussa (kulia), akisalimiana na Balozi Mdogo kutoka Falme za Kiarabu wakati wa hafla ya Mkuu wa Mkoa Paul Makonda kutoa msaada wa vyakula kwa masheikh wa mkuo huo leo. (Katikati) ni Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda.
Baadhi ya Masheikh waliofika katika hafla hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Mhe. Paul Makonda leo amewakabidhi shehena ya viungo vya kutengeneza futari  kwa  maimamu, mashehe na viongozi wa Dini ya Kislamu kutoka Misikiti zaidi ya 1,000 kama sehemu ya sadaka na shukrani ya Amani na Utulivu ndani ya mkoa huo.


Miongoni mwa vitu alivyokabidhi RC Makonda ni Mchele, Sukari, Unga, Maharage, Mafuta na vitu mbalimbali kwaajili ya kuwawezesha viongozi hao kufurahia futari majumbani mwao.

RC Makonda  amewashukuru viongozi wa dini kwa kuwa wasimamizi wazuri wa  Amani na mshikamano ndani ya mkoa huo jambo linalofanya mkoa huo kuendelea kuwa  kisima cha Amani.

Hata hivyo RC Makonda amewaeleza Viongozi wa Dini kuwa namna bora ya kumuunga mkono Rais Dkt. John Magufuli na kumuombea ni kuhakikisha waumini wao wanajiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili wachague viongozi wa serikali za mitaa wanaochukia Rushwa.

Aidha RC Makonda  amemshukuru Balozi wa Falme za Kiarabu kwa kumkabidhi misaada hiyo huku akiwasihi waislamu kutumia mfungo huu  Kuliombea taifa na viongozi pamoja na kuwahimiza wazazi kuwalea watoto katika malezi bora.

Kwa upande wake Balozi mdogo wa Falme za Kiarabu amesema wameamua kumuunga mkono RC Makonda kwakuwa wanamuamini akipokea kitu kinawafikia walengwa na amekuwa mtu wa kuwasaidia watu wasiojiweza bila kujali dini wala kabila.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages