Jeshi la Polisi leo limetoa onyo kali kwa kikundi kinachohamasisha
maandamano ya kuiangusha Serikali kupitia mtandao wa Telegram ambapo
limesema kuwa kitendo hicho ni sawa na uhaini.
Akizungumza na vyombo vya habari leo Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo
wa jeshi hilo, Nsato Marijani amesema kwamba kumekuwa na kikundi ambacho
kinatumia mtandao huo kuhamasisha maandamano kinyume cha sheria na
kutaka kwenda hadi Ikulu kufanya watakayo.
"Sisi kama jeshi la polisi tunawataka kufanya mambo kwa mujibu wa sheria
na siyo vinginevyo kwani kitendo cha kufanya maandamano ukiwa na nia ya
kuiondoa serikali ni Uhaini. Hatua kali zitachukuliwadhidi ya watu
watakaovunja sheria na tusije kulaumiwa kwa lolote," Kamanda Nsato.
Hata hivyo amesema kuwa anaamini wengi wanaopanga mipango hiyo ni vijana
na anaamini kuwa wengi wao wameingia huko kwa kufuata mkumbo na kutaka
wazazi wachukue nafasi zao kuwaonya watoto wao.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, March 9, 2018
Polisi yatoa onyo kwa wanaomasisha kuiangusha serikali
Tags
KITAIFA#
Share This
About kilole mzee
KITAIFA
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment