Wanafunzi wa darasa awali hadi la sita katika Shule ya Msingi Raha Leo
Elimu Maalumu (viziwi) Manispaa ya Mtwara Mikindani wanasoma katika
darasa moja, kutokana na kukosekana kwa vyumba vya madarasa.
Pia, darasa hilo linalotegemewa na wanafunzi 25 linatumika kama ofisi ya walimu, stoo na bwalo.
Hayo yameelezwa leo Ijumaa Machi 9 , 2018 na kiongozi wa wanafunzi hao,
Twaha Salum wakati wa kupokea zawadi kutoka kwa wanawake wafanyakazi wa
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Tawi la Mtwara, kama sehemu ya maadhimisho
ya Siku ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa jana.
Twaha amedai kila wanapotembelewa na wageni wamekuwa wakiwaeleza
changamoto zinazowakabili ili kuwatafutia utatuzi lakini inashindikana.
“Darasa hili linatumika na wanafunzi wote wa elimu maalumu, ndiyo stoo,
ofisi ya walimu wetu na tunalitumia kama. Changamoto ni nyingi kila
wakija wageni tunawaambia lakini hakuna kinachofanyika,”amesema Twaha.
Mwalimu wa kitengo hicho, Caroline Chitunda amesema mbali na changamoto
zilizotajwa na mwanafunzi huyo, wanakabiliwa na ukosefu wa bweni na
chumba maalumu kwa ajili ya kupimia usikivu wa wanafunzi licha ya
kupatiwa vifaa vyote.
“Kama mnavyoona meza moja wanasomea madarasa mawili mawili. Pia tuna
uhaba wa vyumba vya madarasa na chumba cha upimaji wa masikio kwa sababu
wanaofika kuanza kusoma hapa lazima apimwe usikivu, ni chumba maalumu
hakitoi sauti na hakiingizi sauti lakini vifaa vyote tunapatiwa na
Serikali,” amesema Chitunda.
Mwalimu mkuu msaidizi, Ally Matola amesema wanafunzi wa madarasa mawili wanatumia mbao moja kwa ajili ya kusoma.
“Mbao moja inatumika wa madarasa mawili,hawa watoto wasio na usikivu
kipindi kimoja kinachukua muda mrefu tofauti na wale wenye usikivu
kamilifu, walimu wanapokezana kufundisha unakuta vipindi kwa siku
havikamiliki,” amesema Mwalimu Matola.
Ofisa Habari wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Jamadi Omari amesema
wanatambua changamoto zinazoikabili shule hiyo na kwa sasa wameanza
kutafuta ufumbuzi wa vyoo kwanza.
“Tunalifahamu lakini manispaa tuna changamoto nyingi na katika Shule ya
Raha Leo tumeanza na vyoo kwanza kwa sababu ni tatizo na tunafanya kwa
awamu kutatua changamoto zilizopo,”amesema Omari.
Wakina mama wa BoT Tawi la Mtwara wamekabidhi sukari, unga, mafuta ya
kula, majani ya chai, biskuti, shuka, maharagwe, mchele na juisi ambazo
fedha zimetokana na kujichanga kwa wafanyakazi wakiwamo wanaume.
Mwenyekiti wa kamati ya kina mama, BoT Tawi la Mtwara, Zakia Juma
ameiomba jamii kujitokeza na kuwatembelea watoto wenye uhitaji maalumu
kwani na wao wanahitaji upendo.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, March 9, 2018
Tatizo la madarasa bado kitendawili Mtwara
Tags
KITAIFA#
Share This
About kilole mzee
KITAIFA
Labels:
KITAIFA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment