A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, January 31, 2018

Ni kweli Serikali Inadaiwa "Waziri Mwijage

"Ni kweli Serikali Inadaiwa "Waziri Mwijage

Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage amekiri ni kweli serikali ya Tanzania inadaiwa na viwanda vya ndani huku akidai wanaosababisha deni lisilipwe ni watanzania wasiolipa kodi.

Waziri Mwijage amebainisha hayo leo (Jumatano) katika mkutano wa Bunge wa 10 kikao cha Pili kinachoendelea kufanyika mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza kwenye wizara yake ambapo aliulizwa kwamba serikali ina mkakati gani madhubuti wa kulipa madeni hayo ili kuweza kunusuru anguko la viwanda ambavyo vimeanzishwa kwa nia njema.

"Kwa niaba ya serikali nasema ndio serikali inadaiwa na sasa tunaongeza jitihada za kuhakikisha kwamba kila stahili ya serikali inakusanywa na kile kitakachokusanywa ndicho tutakachowalipa wale", alisema Waziri Mwijage. 

Pamoja na hayo Waziri Mwijage aliendelea kwa kusema "hatujawalipa wale kwa sababu nasi hatujalipwa, kuna watu hawapendi kulipa kodi na Tanzania tunafanya vibaya kwa sababu kuna watu hawataki kulipa kodi lakini katika nchi nyingine huwezi kupewa haki nyingine hata kuchumbia kama huwezi kuonyesha 'tax clearance'".

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages