A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Saturday, September 30, 2017

SERIKALI YAPOKEA MSAADA WA MASHINE KUTOKA WRATZ.

#1
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na waandishi wa habari (Hawapo kwenye picha) mapema leo jijini Dar es salaam wakati wa tukio la kupokea mashine ya kutoa dawa ya usingizi kutoka kwa taasisi ya Utepe mweupe, pembeni ni Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu.
#2
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akipokea msaada wa mashine ya kutoa dawa ya usingizi  kutoka kwa Mratibu wa Utepe Mweupe Bi.Rose Mlay wakati wa  tukio lililofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.
#3
Picha ya pamoja ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati wa tukio la kupokea mashine ya kutoa dawa ya usingizi kutoka kwa taasisi ya Utepe mweupe lililofanyika mapema leo katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya jijini Dar es salaam.
#4
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akiongea na waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) wakati wa kupokea msaada wa mashine ya kutoa dawa ya usingizi kutoka kwa taasisi ya Utepe mweupe mapema leo jijini Dar es salaam, pembeni ni Mratibu wa Utepe Mweupe Bi.Rose Mlay.
NA NOEL RUKANUGA
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imepokea msaada wa mashine ya kutoa usingizi wakati wa upasuaji yenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 60 kutoka Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama (WRATZ).

Akipokea msaada huo Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu, amesema kuwa mashine hiyo itakuwa na msaada mkubwa katika ikupunguza vifo vya watoto na akina mama wakati wa kujifungua.

Amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu zimebainisha kuwa wanawake 30 hufariki kila siku jambo ambalo sio rafiki kwa taifa.

Mhe. Ummy amesema kuwa katika kuhakikisha wanaboresha mazingira ya huduma za afya kwa wazazi na watoto, serikali imejipanga kabla ya mwezi Juni mwakani kuongeza vituo 170 vya kutoa huduma ya uzazi.

Amefafanua kuwa serikali imetenga sh.bilioni 8 kwa ajili ya kununua vifaa pamoja na dawa kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ili kukabiliana na vifo vya akina mama na watoto.


Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa mashine hiyo inauwezo wakutengeneza asilimia 21 ya hewa ya oksijeni kwa ajili ya kumsaidia mgonjwa.

Dk. Ulisubisya amesema kuwa mashine hiyo inawezo mkubwa kutokana inaweza kufanya kazi bila kutumia umeme wa kawaida.

“Umeme unapokatika ina uwezo wakutumia hewa ya oksijeni ya kawaida ambayo inatumiwa na watu wengine” amesema Dk. Ulisubisya.

Ameeleza kuwa msaada huo ni hatua kubwa katika maendeleo ya uboreshwaji wa huduma za afya nchini, kinachotakiwa kwa sasa ni kuandaa wataalamu wakutumia mashine hiyo.


Naye Mratibu wa Taifa wa WRATZ Rose Mlay, amesema kuwa ni kuhakikisha wanaokoa maisha ya wazazi na watoto wakati wa kujifungua.

Amesema wameona ni vema kufanya hivyo ili kuhakikisha katika sekta ya afya inasonga mbele na kuwa na mafanikio.

“Mashine hii itatumika kusaidia kuokoa maisha ya mama na mototo na watu wengine” amesema Mlay.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages