Akizungumza
kwenye Ghala la kuhifadhia vifaa vya ujenzi wa Ofisi hizo lililopo
kwenye Kambi Mama ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT Mgulani RC Makonda
ameishukuru Bank ya CRDB kwa kutoa fedha zilizofanikisha kupatikana kwa
mifuko hiyo.
Aidha
amesema Bank ya CRDB pia imejitolea kuweka Dawati maalumu kwenye kila
Tawi la Bank hiyo kwaajili ya wananchi wanaotaka kuchangia Ujenzi wa
Ofisi za Walimu ambapo Mwananchi anaweza kuchangia kiasi chochote cha
Fedha ambapo wengine wataweza kuchangia kwa SimBank
Amesema
kuwa kazi ya ujenzi wa Ofisi za kisasa za Walimu iyafanyika Usiku na
Mchana chini ya Vijana wenye morali ya kufanya kazi kutoka JKT,Jeshi la
Magereza na Jeshi la Polisi ambao Wamemuunga Mkono RC Makonda.
Makonda
amewapongeza wadau waliomuunga mkono na wanaoendelea kumuunga mkono
katika kufanikisha kampeni hiyo ambapo amewaomba Wananchi kumuunga
mkono.
Amesema
kuwa hadi sasa amefanikiwa kupata wadau walioahidi kufunga miundombinu
ya vifaa vyote vya umeme ikiwemo Taa, Feni ambapo wengine wametoa Mabati
10,000 huku wengine wamejitolea kuweka Vifaa vyote vya Vyoo.
No comments:
Post a Comment