Mashindano ya Mbio za Baiskeli katika Mikoa mitano ya Kanda ya
ziwa yanataraji kufanyika AGOSTI 6, 2017 katika Viwanja vya Halmashauri ya Mji
wa Bariadi, Mkoani Simiyu.
Mashindano hayo yameandaliwa na Kampuni ya uzalishaji wa
Vinywaji Baridi ya JAMBO FOOD PRODUCT kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
wa Simiyu.
Mashindano hayo yatahusisha Umbali wa Kilomita 200 kwa Wanaume,
Kilomita 80 kwa Wanawake na Kilomita 5 kwa watu wenye Ulemavu.
Pia kutakuwa na Burudani Mbalimbali Kutoka kwa WAGIKA na WAGARO
na Ngoma nyingine nyingi za Asili zitatolewa siku hiyo. Zawadi Mbalimbali
zitatolewa kwa washiriki ikiwemo Pikipiki na fedha Taslimu zaidi ya Shilingi
Milioni nane.
Fomu za Ushiriki wa SIMIYU JAMBO FESTIVAL 2017 zinapatikana
katika Ofisi za Maafisa Michezo katika Halmashauri za Mikoa ya Shinyanga,Simiyu,Geita, Mwanza, kwa Gharama ya Shilingi 5000 tu.
Mgeni rasmi Katika Mashindano hayo ya mbio za Baiskeli ya SIMIYU
JAMBO FESTIVAL 2017 atakuwa Naibu Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Tulia Ackson.
Mkoa wa Simiyu, Wilaya Moja Bidhaa Moja.
HAKUNA KIINGILIO WOTE MNAKARIBISHWA
No comments:
Post a Comment