Mwenyekiti
wa Chama Cha Alliance For Democratic Change (ADC), Mdoe Hassan akizungumza na waandishi wa habari katika
viwanja vya ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dar-es-salaam Paul Makonda jana
walipokwenda kumuomba Rais Dkt.John Magufuli alegeze masharti ya mikutano ya
siasa nchini.
Na Yusuph Mlandula
Chama Cha ADC chamuomba Rais JPM kulegeza masharti ya siasa.
Chama cha Alliance For Democratic Change (ADC) kimemuomba
Rais Dkt. John Magufuli kulegeza masharti aliyoyaweka katika siasa ili waweze
kufanya mikutano ya hadhara ambayo itasaidia wanachama wao kujua mipango ya
chama.
Hayo yamesemwa mapema hii leo jijini Dar es salaam na Katibu
Mkuu wa Chama hicho, Doyo Hassan Doyo mara baada ya kufanya ziara katika ofisi
za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam. Paul Makonda.
Amesema kuwa shughuli za siasa ni haki ya kila chama
kikatiba kwani kuzuia shughuli hizo ni kubinya uhuru na taratibu zilizoelekezwa
na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, Chama hicvho kinaadhimisha miaka mitano tangu
kianzishwe kwa kufanya ziara ya kutemblea vyombo vya habari mbalimbali
ili kuweza kutoa ushirikiano na kujitangaza hasa katika kuelezea mafanikio
waliyoyapata.
No comments:
Post a Comment