Mkuu
wa Masoko wa Benki ya DTB, Sylvester Bahati (kushoto), akizungumza na waandishi
wa habari katika uzinduzi wa kampeni ya Chakarika inayowasidia
wateja wajasiriamali kuwaongezea ufanisi kwenye biashara kwa kuwafungulia fursa
mbalimbali kupitia akaunti zao. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam leo.
Katikati ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTB, Viju Cherian na Mkuu wa Idara ya Huduma
za kibenki wa benk hiyo, Kumar Dandapani.
Taarifa kwa Umma
Kampeni ya
Chakarika
Benki
ya Diamond Trust Bank Tanzania leo hii imezindua “Chakarika Campaign” ambayo ni
kampeni mahususi iliyobuniwa katika kuwaongezea wajasiriamali ufanisi kwenye
biashara zao kwa kuwafungulia fursa mbali mbali kupitia Akaunti ya Biashara.
Kama neno “Chakarika” lisemavyo Akaunti hii ya Biashara imeundwa kwa
wajasiriamali wachakarikaji wenye malengo ya kukuza na kufanikiwa katika
biashara zao.
Kampeni
ya Chakarika inalenga kuhamasisha wajasiriliamali wanaochipukia kuacha kutumia
akaunti zao binafsi katika kufanya miamala ya kibiashara na kufungua Akaunti
hiyo ya Biashara. DTB Tanzania imeboresha Akaunti ya Biashara kwa kupunguza
kiwango cha kufungulia akaunti hiyo hadi TSHs 50,000 na kupunguza makato ya
kila mwezi mpaka TSHs 12,000 kwa mwezi. Kampeni hiyo pia itatoa fursa kwa kila
anayefungua Akaunti ya Biashara kushinda zawadi mahususi katika kipindi kizima
cha Kampeni hiyo.
Ndani
ya miaka 9, DTB Tanzania imeweza kupanda katika nafasi ya 5 kutoka nafasi ya
kumi kwa ukubwa wa Amana za Wateja kati ya mabenki zaidi ya 50 nchini. Ndani ya
muda huu DTB Tanzania pia imefanikiwa kukuza mtandao wao wa matawi kutoka
matawi 6 tu mpaka matawi 28 nchini, 14 kati ya hayo yakiwa jijini Dar es
Salaam.
Fursa
kwa wajasiriamali zinazopatikana kupitia kampeni hii ni pamoja na fursa ya
kukuza mitaji, uhifadhi wa kumbukumbu za biashara pamoja na uwezo wa kufanya
miamala ya kibashara kwa wakati. Akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi wa
Kampeni hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa DTB Tanzania, Ndugu Viju Cherian alisema,
“Mafanikio makubwa ya DTB Tanzania ndani ya miaka 9
iliyopita yametokana na jitihada za watendaji chipukizi walio makinikatika
kutoa huduma.” DTB inajivunia kuwa watendaji ambao wamepitia mafunzo maalum ya
kunoa ujuzi katika maswala ya kibenki na ya huduma kwa wateja.
Ndugu
Cherian aliongeza kwa kusema, “Kutoa huduma bora kwa haraka ni tamaduni yetuhivyo
kuwapa wateja wetu muda wa kufanya mambo mengine yenye tija zaidi yakiwemo
kukuza biashara zao na kutumia muda na ndugu na marafiki.” Pamoja na matawi 28
yaliyotapakaa nchi nzima, DTB Tanzania pia inatoa huduma kwa njia mbadala
kupitia Internet Banking, Mobile Banking pamoja na mtandao wa mashine za ATM.
“Dhamira
yetu kubwa kama benki ni kutoa huduma zilizo kamilika, huduma zinazotosheleza
mahitaji ya kila mteja bila kujali umri, jinsia au hali yao ya kifedha. Sisi ni
Benki ya kila Mtanzania na hii inaonekana dhahiri katika huduma tunazotoa.
Kupitia Kampeni ya Chakarika, ningependa kuwakaribisha wajasiriamali wote,
waliobobea na wanaochipukia kutembelea matawi yetu na kufungua akaunti nasi.”
aliongeza Ndugu Cheria.
DTB
Tanzania kwa sasa ina matawi 28 nchini, 14 kati ya hayo yakiwa jijini Dar es
Salaam kama ifuatavyo (Mtaa wa Jamaat, Masaki, Morocco, Magomeni, Mbezi,
Mbagala, Nyerere, Kariakoo, Tawi la Nelson Mandela, Upanga lililo barabara ya
Umoja wa Mataifa na Tawi la CBD lililo kwenye makutano ya barabara za Samora na
Mirambo) jingine ni Tawi Mbezi Chini lililo Kata ya Kawe na tawi jipya kabisa
la Mlimani City. Matawi mengine yakiwemo matawi mawili kwa miji ya Mwanza na
Arusha na tawi moja katika miji ya Dodoma, Kahama, Mbeya, Morogoro, Moshi,
Mtwara, Mwanza, Tabora, Tanga na visiwa vya Zanzibar.
DTB
Tanzania ni kampuni tanzu ya makampuni ya DTB (DTB Group) yanayoendesha
shughuli za kibiashara katika ukanda wa
Africa Mashariki nchini Kenya, Uganda na Burundi. DTB Tanzania pia ni kampuni
tanzu ya Mfuko wa Aga Khan wa Maendeleo ya Kiuchumi (The Aga Khan Fund for
Economic Development – AKFED) ambayo ni tawi la Mtandao wa Maendeleo wa Aga
Khan (Aga Khan Development Network -AKDN)
No comments:
Post a Comment