A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, July 24, 2017

DTB YAZINDUA CHAKARIKA KAMPENI



Mkuu wa Masoko wa Benki ya DTB, Sylvester Bahati (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa kampeni ya  Chakarika inayowasidia  wateja wajasiriamali kuwaongezea ufanisi kwenye biashara kwa kuwafungulia fursa mbalimbali kupitia akaunti zao. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa DTB, Viju Cherian na Mkuu wa Idara ya Huduma za kibenki wa benk hiyo, Kumar Dandapani.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya DTB,  Cherian (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya  Chakarika itakayowasidia  wateja wajasiriamali kuwaongezea ufanisi kwenye biashara kwa kuwafungulia fursa mbalimbali kupitia akaunti zao. Uzinduzi huo ulifanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Masoko, Sylevester Bahati na  Mkuu wa Idara ya Huduma za kibenki wa benki hiyo, Kumar Dandapani. 




Taarifa kwa Umma
Kampeni ya Chakarika

Benki ya Diamond Trust Bank Tanzania leo hii imezindua “Chakarika Campaign” ambayo ni kampeni mahususi iliyobuniwa katika kuwaongezea wajasiriamali ufanisi kwenye biashara zao kwa kuwafungulia fursa mbali mbali kupitia Akaunti ya Biashara. Kama neno “Chakarika” lisemavyo Akaunti hii ya Biashara imeundwa kwa wajasiriamali wachakarikaji wenye malengo ya kukuza na kufanikiwa katika biashara zao.


Kampeni ya Chakarika inalenga kuhamasisha wajasiriliamali wanaochipukia kuacha kutumia akaunti zao binafsi katika kufanya miamala ya kibiashara na kufungua Akaunti hiyo ya Biashara. DTB Tanzania imeboresha Akaunti ya Biashara kwa kupunguza kiwango cha kufungulia akaunti hiyo hadi TSHs 50,000 na kupunguza makato ya kila mwezi mpaka TSHs 12,000 kwa mwezi. Kampeni hiyo pia itatoa fursa kwa kila anayefungua Akaunti ya Biashara kushinda zawadi mahususi katika kipindi kizima cha Kampeni hiyo.


Ndani ya miaka 9, DTB Tanzania imeweza kupanda katika nafasi ya 5 kutoka nafasi ya kumi kwa ukubwa wa Amana za Wateja kati ya mabenki zaidi ya 50 nchini. Ndani ya muda huu DTB Tanzania pia imefanikiwa kukuza mtandao wao wa matawi kutoka matawi 6 tu mpaka matawi 28 nchini, 14 kati ya hayo yakiwa jijini Dar es Salaam.

Fursa kwa wajasiriamali zinazopatikana kupitia kampeni hii ni pamoja na fursa ya kukuza mitaji, uhifadhi wa kumbukumbu za biashara pamoja na uwezo wa kufanya miamala ya kibashara kwa wakati. Akiongea na wanahabari wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa DTB Tanzania, Ndugu Viju Cherian alisema, “Mafanikio makubwa ya DTB Tanzania ndani ya miaka 9 iliyopita yametokana na jitihada za watendaji chipukizi walio makinikatika kutoa huduma.” DTB inajivunia kuwa watendaji ambao wamepitia mafunzo maalum ya kunoa ujuzi katika maswala ya kibenki na ya huduma kwa wateja. 


Ndugu Cherian aliongeza kwa kusema, “Kutoa huduma bora kwa haraka ni tamaduni yetuhivyo kuwapa wateja wetu muda wa kufanya mambo mengine yenye tija zaidi yakiwemo kukuza biashara zao na kutumia muda na ndugu na marafiki.” Pamoja na matawi 28 yaliyotapakaa nchi nzima, DTB Tanzania pia inatoa huduma kwa njia mbadala kupitia Internet Banking, Mobile Banking pamoja na mtandao wa mashine za ATM.


“Dhamira yetu kubwa kama benki ni kutoa huduma zilizo kamilika, huduma zinazotosheleza mahitaji ya kila mteja bila kujali umri, jinsia au hali yao ya kifedha. Sisi ni Benki ya kila Mtanzania na hii inaonekana dhahiri katika huduma tunazotoa. Kupitia Kampeni ya Chakarika, ningependa kuwakaribisha wajasiriamali wote, waliobobea na wanaochipukia kutembelea matawi yetu na kufungua akaunti nasi.” aliongeza Ndugu Cheria.


DTB Tanzania kwa sasa ina matawi 28 nchini, 14 kati ya hayo yakiwa jijini Dar es Salaam kama ifuatavyo (Mtaa wa Jamaat, Masaki, Morocco, Magomeni, Mbezi, Mbagala, Nyerere, Kariakoo, Tawi la Nelson Mandela, Upanga lililo barabara ya Umoja wa Mataifa na Tawi la CBD lililo kwenye makutano ya barabara za Samora na Mirambo) jingine ni Tawi Mbezi Chini lililo Kata ya Kawe na tawi jipya kabisa la Mlimani City. Matawi mengine yakiwemo matawi mawili kwa miji ya Mwanza na Arusha na tawi moja katika miji ya Dodoma, Kahama, Mbeya, Morogoro, Moshi, Mtwara, Mwanza, Tabora, Tanga na visiwa vya Zanzibar.



DTB Tanzania ni kampuni tanzu ya makampuni ya DTB (DTB Group) yanayoendesha shughuli  za kibiashara katika ukanda wa Africa Mashariki nchini Kenya, Uganda na Burundi. DTB Tanzania pia ni kampuni tanzu ya Mfuko wa Aga Khan wa Maendeleo ya Kiuchumi (The Aga Khan Fund for Economic Development – AKFED) ambayo ni tawi la Mtandao wa Maendeleo wa Aga Khan (Aga Khan Development Network -AKDN)

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages