DC SOPHIA MJEMA APONGEZA JITIHADA ZINAZOFANYWA NA CHUO CHA ST.MARK KATIKA KUELIMISHA JAMII
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akizungumza na wanajumuiya ya Chuo
cha St. Mark kilichopo Buguruni Malapa alipofanya ziara ya kikazi chuoni
hapo.Kulia kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Dr. Peter Kopweh na kushoto ni
Mshauri wa majeshi ya akiba Chripin Makota.
Wanajumuiya ya Chuo cha St. Mark kilichopo Buguruni Malapa wakimsikilia Mh.Sophia Mjema alipofanya ziara ya kikazi chuoni hapo.
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akianza ziara kukagua maeneo
mbalimbali yanayokizunguuka chuo cha St.Mark akiwa
ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama pamoja na timu ya wataalamu
wa wilaya ya Ilala.
Kaimu
Mkuu wa Chuo cha St. Mark Dr.Peter Kopweh akifafanua jambo mbele ya Mkuu
wa wilaya alipokuwa akizuru maeneo mbalimbali katika chuo hicho.
Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa
Mipango Miji Ilala Bw. Benjamin Chagula wakati akiangalia namna ya
kutatua Changamoto ya mipaka ya chuo hicho inaingiliwa na wananchi
wanaoishi eneo jirani.
Na Yusuph Mlandula
Nae
katika hotuba yake Mh.Mjema ambaye alipata fursa ya kuzungukia maeneo
kadhaa chuoni hapo alieleza lengo kuu la kufika chuoni hapo kadhalika
kupongeza uongozi wa chuo hicho kwa jitihada zinazofanyika.
“Nimeamua
kutoka na kuja kuwaona kwani nauthamini sana uwepo wenu katika wilaya
yangu (Ilala) kwani hii ni fursa muhimu ya serikali kuwatumia wasomi
hata waliopo vyuoni kutatua Changamoto katika maeneo waliyopo, mimi
nakazia hapa wilayani na naamini ujio huu utakuwa wenye tija sana kwetu
sisi pamoja nanyi kama taasisi katika kushirikiana” alisema Mh. Sophia
Mjema.
Kadhalika
akizungumza na wanafunzi pamoja na wafanyakazi wa chuo hicho, Mh.Mjema
alitangza kufungua milango ya fursa kwa wasomi hao kufika ofisini kwake
na kuleta mawazo pamoja na nguvu zao ili kusukuma gurudumu la maendeleo
mbele huku akikazia suala la uzalendo pamoja na wito wa Mh Rais Magufuli
kuhusu kufanya kazi.
Vilevile
Mh. Mjema alikazia suala la kuimarisha misingi ya elimu ya juu kwa
kuwekeza kwenye uboreshaji wa teknolojia kwani dunia ya sasa mitandao
umekuwa nyenzo muhimu ya kupata taarifa za kitaaluma.
“Mkakati
wa kusambaza huduma ya intaneti (WIFI) katika vyuo vikuu hapa Ilala
unaendelea kwa kasi na umesimama kwa muda kutokana na hali ya mvua
lakini baada ya hali hii kila kitu kitakuwa kama ilivyoahidiwa,lazima
msome kisasa” alihitimisha.
Nae
Rais wa chuo kwa niaba ya wanafunzi wote alifikisha Changamoto
zinazowakabili ikiwemo suala la mikopo pamoja na tatizo la kukatika kwa
umeme mara kwa mara kwani limekuwa likidhohofisha maendeleo ya taaluma
alitoa shukrani kwa mkuu wa wilaya na kuahidi ushirikiano na ofisi ya
wilaya pamoja na kujitoa kutumia taaluma zao ndani ya jamii kwa ujumla.
Akihitimisha
zoezi hili pamoja na kumshukuru Mh.Mjema kwa kufika chuoni hapo, Kaimu
Mkuu wa Chuo alitoa wito kwa watanzania kujiunga na Chuo hicho hasa
wakati huu ambapo milango ipo wazi kwa wanafunzi kudahiliwa vyuoni moja
kwa moja huku akiwaondoa hofu wale wanaobanwa na kazi kuwa watapata
fursa ya kusoma masomo ya jioni.
No comments:
Post a Comment