Kamati ya uongozi ya Chama cha ACT
Wazalendo inatarajia kukutana leo juni 7 kutafakari namna ambayo
mwenyekiti wao wa chama Anna Mghwira ambavyo atatekeleza wajibu wake katika
chama hicho na majukumu mapya aliyoyapata.
Akitoa taarifa hiyo Katibu wa
itifaki na Uenezi na mawasiliano ya umma wa ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema
chama hicho kimepokea taarifa kuhusu uteuzi wa mwenyekiti wao wa chama
hicho kuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro.
"Taarifa za Mwenyekiti wa chama
chetu kuwa mkuu wa mkoa wa kilimanjaro uteuzi usika umefanyika wakati mama
Mghwira akiwa nje ya nchi na baada ya kurejea amefanya mazungumzo na viongozi
wenzake wa juu wa chama kuhusu uteuzi wake" alisema Shaibu.
Chama hicho kimewataka wanachama
wake kuwa na utulivu wakati wa vikao vya chama vinavyochukua hatua stahiki
kuhusu jambo hilo.
June 3, 2017 Rais Magufuli
alimteua Mwenyekiti wa Taifa Chama cha ACT Wazalendo, Anna Elisha Mghwira kuwa
Mkuu mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro.
No comments:
Post a Comment