Mwanamume huyo
aliwashambulia wageni hao katika mgahawa wa Lukman Mkunazi Mjini Zanzibar.
Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali aliwaambia waandishi wa
habari Jumatatu kuwa mtuhumiwa aliyetenda hayo hayatambuliwa kwa jina.
Hata hivyo,
anafahamika kwa sura na, anakisiwa kuwa na umri wa miaka 25.
Bw Ali alisema
uchunguzi wa awali umebaini mtuhumiwa huyo alifika katika mgahawa huo na
kuwachoma watu watatu ambao walikuwa mgahawani hapo kwa ajili ya kujipatia
chakula na kisha akakimbia na akiwa njiani akawashambulia wengine watatu.
Walioshambuliwa ni
Mauget Gerarol ambaye ni raia wa Ufaransa, Liying Liang raia wa Canada na
Jennifer Wolf na Anna Catharina ambao ni raia wa Ujerumani.
Wengine ni Hassan
Abdallah na Sajad Hussein.
Kwa mujibu wa gazeti
la Mwananchi, Bw Ali alisema majeruhi wote walipatiwa matibabu na kuruhusiwa
lakini Mauget Gerarol raia wa Ufaransa bado amelazwa hospitalini.
Zanzibar hutegemea
sana utalii.
No comments:
Post a Comment