A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, August 11, 2022

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AIPONGEZA BENKI YA CRDB, AHITIMISHA MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Serikali kubuni mfumo wa kidigitali utakaoiwezesha Wizaya ya Kilimo kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) kuagiza mbolea na kuisambaza kwa mkulima, hivyo ruzuku itolewayo na Serikali kumfikia mnufaika kama ilivyokusudiwa.

Mhe. Rais ametoa pongezi hizo jana alipohitimisha rasmi Maonyesho ya wakulima Nanenane katika Viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya. Mhe. Rais amezitaka taasisi za fedha na benki za biashara nchini kuendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha sekta ya kilimo inapewa kipaumbele.

“Aidha, nazipongeza benki nchini kwa kushiriki vyema katika kuhakikisha sekta ya kilimo inakua na kuleta tija nchini, niipongeze Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Serikali kufanikisha mfumo huu kwani naamini utaleta mapinduzi makubwa ya kilimo nchini,” alisema Rais Samia.

Benki ya CRDB imekuwa kinara katika kuhakikisha inashirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wadau wa sekta za kilimo, uvuvi, mifugo, misitu, biashara na viwanda ikiongozwa na kaulimbiu yake isemayo “Kilimo chetu, Viwanda vyetu, Uchumi Wetu” hivyo kuongeza tija ya uwekezaji kwenye sekta hizo ikizingatiwa umuhimu wa kuunganisha wateja wote kwenye mnyororo wa thamani katika uzalishaji ili kuwapatia uhakika wa masoko ya bidhaa zao.


Mkurugenzi Mtendaji Abdulmajid wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alielezea namna benki hiyo ya kizalendo imekuwa mdau mkubwa wa sekta zote za kiuchumi nchini kwa kuwasaidia wakulima, wafugaji au wavuvi iwe mmojammoja, vikundi, vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS), wakulima wakubwa, wafanyabiashara wa mazao ya kilimo na wawekezaji kwenye viwanda vinavyoongeza thamani ya malighafi zinazozalishwa nchini.

“Kiujumla zaidi ya 43% ya mikopo yote itolewayo kwa ajili ya kilimo nchini imetolewa na Benki ya CRDB. Kwa mwaka 2021/2022, tumetoa zaidi ya shilingi bilioni 769. Sehemu kubwa ya mikopo itolewayo na Benki ya CRDB imeelekezwa katika kilimo cha mazao ya biashara, kilimo cha mazao ya chakula, uvuvi, mifugo, uzalishaji wa malighafi za viwanda, ujenzi wa viwanda vya uchakataji wa mazao ya kilimo, utengenezaji wa pembejeo, uendelezaji wa mazao ya misitu, usindikaji na usambazaji,” alisema Nsekela.


Kwa kipindi cha miaka mitano ilyopita hadi Juni 2022, alisema Benki ya CRDB imetoa mikopo kwenye sekta ya kilimo kiasi cha TZS 2.6 Trilioni. Ikumbukwe CRDB ilikuwa benki ya kwanza nchini kutoa mikopo kwa riba ya tarakimu moja ikitoza asilimia 9 katika sekta ya kilimo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages