A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, July 17, 2022

MBUNGE SEGEREA AHIMIZA WANANCHI KUHUSU SENSA YA WATU NA MAKAZI


MBUNGEwa Jimbo la Segerea, wilayani Ilala, mkoani Dares Salaam, Bonnah Kamori, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki  Sensa ya Watu na Makazi, inayotarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu  ili kuunga mkono  jitihada za  Rais Samia Suluhu Hassan kuwaletea maendeleo.

Aliyasema hayo, jana, katika matembezi  maalumu  aliyoyandaa ya kuhamasisha Sensa ya Watu na Makazi  pamoja na kumpongeza Rais Samia.

Mbunge Bonnah  alieleza,  Sensa ya Watu na Makazi ni muhimu kwa maendeleo ya jimbo hilo na taifa kwa ujumla kwani  inairahisishia serikalikuandaa mipango  yake ya maendeleo.

“Tukihesabiwa  itasaidia serikali kupanga bajeti sahihi ya maendeleo kulingana na idadi yawatu. Sensa hii nimuhimu kwa wananchi wa  Jimbo la Segerea kwa sababu jimbo hili ndiyo lenye wananchi wengi.

Tanzania nzima, hivyo tukijitokeza kwa wingi  ninaamini itasaidia serekali kutuletea maendeleo,”alisema Bonnah.

Alibainisha,  sensa  itarahisisha  serikali kupanga bajeti  sahihi kaika kujenga miundombinu bora ya elimu, huduma za afya,barabara, maji na shughuli mbalimbali za maendeleo, hivyo kuwaomba wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi Agosti 23 kuhesabiwa.

Aliishukuru serikali chini ya  Rais Samia kwa kasi kubwa ya maendeleo hapa nchini, kufungua fursa za kiuchumi, kitaifa na kimataifa pamoja na kuwawezesha wananchi kupitia fursa mbalimbali   ikiwemo ya mikopo ya asilimia 10  isyo na riba inayotolewa na Halmashauri  kwa vikundi vyawajasiriamali wanawake, vijana nawatu wenye ulemavu.

Pia kupitia Filamu ya Tanzania The Royal Tour ambayo alisema imekuwa fursa muhimu ya maendeleo kwa taifa.

Matembezi hayo yalipita katika mitaa mbalimbali ya Kata ya Kiwalani,  huku yakihudhuriwa na madiwani wa kata mbalimbali za Halmashauri ya Jiji la Dares  Salaam, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilala na  wananchi  kutoa ndani na nje ya jimbo hilo.

Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Ilala, Said Side, alimpongeza Mbunge Bonnah kwa kuandaa matembezi hayo na kueleza kuwa ufanisi katika Sensa ya Watu na Makazi,  utaisaidia serikali chini ya Rais Samia katika utekelezaji wa Ilani ya Chama. 

“Wananchi wa Jimbo la Segerea nawaombeni sana. Agosti 23 mwaka huu tujitokeze  kuhesabiwa. Ni muhimu kwa maendeleo ya taifa letu. Tunamshukuru Mbunge wetu Bonnah kwa kuliona hili na kuamua kuandaa matembezi haya,”alisema Side.

Diwani wa Viti Maalumu, Betrice  Edward, alisema Sensa yaWatu na Makazi ni msingi wa maendeleo kwa taifa lolote katika kuandaa bajeti sahihi hivyo Agisti 23  wananchi wote wanapaswa kushiriki katika sensa.

Aprili 8 mwaka huu, Rais Samia alitangaza rasmi  Agosti 23 mwaka huu kuwa Siku ya Sensa yaWatu na Makazi alipokuwa akizindua nembo maalumu ya sensa  visiwani Zanzibar.
Tanzania ilifanya  Sensa ya Watu na Makazi mara mwaka 2012.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages