Vijana
 nchini  wametakiwa kubadilika kifikra kwa kusoma vitabu mbalimbali  
vitakavyowajenga katika maadili  na kufanya Taifa liwategemee katika 
kuleta maendeleo .
 Kusoma vitabu  kusoma vitabu kutafanya 
kuondokana na utumwa wa kifikra na kuwa vijana wanaoweza   kusimamia 
ndoto zao za maisha huku wakikombolewa na umasikini.
Akizungumza 
jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kitabu chake Kiitwacho Vijana
 wa Kikristo na Changamoto na Utatuzi Wake, Mwandishi wa Kitabu hicho 
Mwijarubi Mwijarubi amesema kuwa vijana wengi hawachukui muda  kusoma na
 kujifunza mambo mengi ya kukabiliana na maisha na changamoto zake hivyo
 kupitia kitabu hicho kitaweza kuwasaidia kupambana nazo na kwa kujenga 
fikra mpya zinaweza kuleta suluhu katika maisha yao.
“Kitabu hiki
 kimegawanyika katika changamoto za vijana katika makundi makuu manne 
ambayo yamefafanuliwa kwa ufupi katika Afya,Uchumi, Utandawazi na 
Mahusiano”. Amesema Mwijarubi.
Kwa upande wake Mchungaji Mstaafu 
 wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Richard Hananja 
amewataka vijana kutumia kitabu  kama sehemu ya kutatua na kupambana na 
changamoto za maisha ambazo wakati wa wa sasa wana vitu vingi 
vinavyowazunguka 
Katika uzinduzi huo Mgeni rasmi  wa  kitabu 
hicho Lello Mmasy ambaye ni Mwandishi wa vitabu kama “Mimi na Rais” 
pamoja na Chochoro za Madaraka amesema kwamba kila kijana atakayesoma 
kitabu hicho kitambadilishia mtanzamo wake katika maisha yake na 
kuongeza kuwa vijana ili waweze kubadilika kifikra lazima wasome vitabu 
kama hivyo ambavyo vina majawabu ya changamoto za vijana.
Amesema
 kuwa maisha yanabadilika kwa kasi hivyo vijana wanatakiwa kuleta 
matokeo chanya ya kufanya vitu tofauti ya kubadilika katika nyanja 
mbalimbali za kusaidia maisha yao yaende kwa kufanya vitu tofauti.
Aidha
 amesema kitabu hicho amekisoma na kugundua kipo katika kubadilisha 
vijana   ambapo wanatakiwa kusoma na kuelewa kilichomo na maisha yao 
katika kutafuta ufumbuzi.
Mgeni Rasmi Lello Mmassy watatu kutoka kushoto na akizindua kitabu cha Kitabu cha Kikristo,Changamoto na Utatuzi Wake katika hafla uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwandishi wa Kitabu cha Vijana wa Kikristo ,Chagamoto na Utatuzi wake Mwijarubi Mwijarubi akizungumza kuhusiana na dhamira ya kitabu hicho kwa vijana kitavyowesha kuwakomboa kifikra ,kilichozinduliwa jijini Dar es Salaam.
Mgeni Rasmi wa Kitabu cha Vijana wa Kikrisro ,Changamoto na Utatuzi Wake Lello Mmasy qkizungumza wakati wa Uzinduzi wa kitabu hicho kilichoandikwa na Mwandishi Mwijarubi Mwijarubi kilichozinduliwa jijini Dar es Salaam.

 
 
 
No comments:
Post a Comment