Balozi wa Korea nchini  Kim  Sun 
Pyo amezindua rasmi  Chumba Cha Kutakasia Vifaa Tiba kilichopo katika 
Hospital ya Rufaa ya Tumbi iliyopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.
Akizungumza
 mara baada ya uzinduzi huo Balozi Pyo alisema kuwa uzinduzi huo 
umefanyika mara  baada ya  kumalizika kwa ukarabati wa majengo hayo  
uliotokana na ufadhili wa Taasisi ya Kikorea inayofahamika kwa jina la 
Korea Foundation for International Healthcare (KOFIH).
Kwa upande
 wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi Amani Malima 
alisema kuwa  Hospital hiyo imeongeza wigo  wa utoaji wa huduma  za Afya
 ambapo hivi sasa inahudumia wagonjwa wengi zaidi wanaofika Hospitalini 
hapo baada ya kupata Rufaa ,wasio na wenye  Rufaa kutoka  ndani na nje 
ya Mkoa wa Pwani.
Mganga Mfawidhi Malima aliongeza kwa kusema 
kuwa Hospital hiyo wanapokea majeruhi wengi wa ajali  kwa kuwa  wako  
pembezoni mwa barabara kubwa iendayo Mikoani.
"Kutokana na  
ongezeko la uhitaji wa vifaa tiba   safi  na salama  vilivyotakaswa  kwa
 kufuata sheria na taratibu za kitabibu , ili kukidhi mahitaji ya 
wagonjwa  ambao ni majeruhi wahitaji wa huduma za upasuaji huduma za 
kusafisha  vidonda na huduma nyingine zinazohusiana na hizo, Uongozi wa 
Hospitali ulifikia hatua  ya kuona  umuhimu wa kuwa na Chumba Cha 
Kutakasia Vifaa ambacho kitarahisisha upatikanaji wa huduma za utakasaji
 wa vifaa kwa wagonjwa ili kupunguza maambukizi"alisema 
 Malima 
alisema kuwa mradi mzima wa kukarabati Chumba Cha Kutakasia Vifaa 
umegharimu kiasi cha Mil 232,560,000 huku vifaa na ukarabati wa vyumba 
vya Kutakasia ukigharimu kiasi cha Mil.52,630,000 na ununuzi wa mashine 
pamoja na kusimika ni Mi.179,930,000.
Wakati
 huohuo Mganga Mkuu w Mkoa wa Pwani  Dkt. Gunini Kamba alisema  
wamemtembeza Balozi Pyo kwenye jengo la watoto njiti ambapo kwa siku 
hupokea watoto kati ya 30 hadi 40 ambao wanazaliwa kabla ya umri  wa 
miezi sahihi ya  kuzaliwa.
"Hapo awali hatukuwa na majengo haya  
ambapo baada ya ukarabati mkubwa uliofanyika sasa  hali ya kutunza 
watoto hawa ambao  almaarufu kama njiti  umekuwa rahisi  na salama kwa 
mama na mtoto"alisema Dkt. Gunini.
 
 
 
No comments:
Post a Comment