A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, March 13, 2022

TARI Naliendele yaeleza Mtwara walivyo na uwanda mpana kustawisha mazao mengine bila kuathiri zao la korosho

 

MKURUGENZI wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo, TARI Naliendele Dkt.Fortunus Kapinga amesema kuwa tekolojia ya Mtwara inaruhusu wakulima wa Mtwara kulima mazao mengi yakiwemo mazao ya bustani, jamii ya kunde na nafaka bila kuathiri kilimo cha zao la korosho.

Hivyo wanaweza kujiongezea kipato kutoka kwenye mazao hayo badala ya kutegemea zao la korosho peke yake.
Dkt.Kapinga alisema kuwa mahitaji ya kiikolojia ni mojawapo ya sababu zinazowafanya washauri zao fulani lipandwe wapi, lini na vipi.

Dkt.Kapinga ameyasema hayo wakati akizungumza na Wanafunzi kutoa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Chuo cha Kilimo Borigaram - Kigamboni walioko kituoni hapo kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo (Field Practical) katika taasisi hiyo.
Wakizungumzia tafiti za kilimo cha mboga na matunda (hotculture) wanafunzi hao wamesema wameshangaa kuona migomba ikistawi na kuzaa kwa wingi na kudai kuwa wakazi wa Mtwara wanaweza kutengeneza kipato kikubwa wakati wakisubiri mavuno ya mazao mengine kama vile Korosho na Ufuta.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages