Meneja
Uhusiano na Elimu kwa Umma wa NSSF, Lulu Mengele akimkabidhi vifaa tiba
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Dkt. Msafiri
Marijani kwa ajili ya kusaidia huduma za afya katika hospitali hiyo.
NSSF imefanya makabidhiano hayo wakati wa kuelekea kilele cha siku ya
Wanawake Duniani Machi 8
Katika
kuelekea kilele cha siku ya Wanawake Duniani Machi 8, baadhi ya
wafanyakazi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakiwa
katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi msaada wa vifaa tiba
katika Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar. NSSF kupitia sera ya
kuchangia na kudhamini imekuwa ikiwajibika katika jamii (CSR) kwa kutoa
misaada katika sekta ya afya, elimu , michezo na jamii kwa ujumla.
Na MWANDISHI WETU
Mfuko
wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa msaada wa vifaa tiba katika
Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar ambavyo ni vitanda vya
kujifungulia pamoja na mashine za kupimia shinikizo la damu ambavyo
vitasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa wanaopata huduma katika hospitali
hiyo.
“NSSF katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Machi 8 na mwaka huu ikiwa na kauli mbiu isemayo ‘Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu’ Mfuko umeamua kusaidia vifaa tiba katika hospitali hii ya Mnazi Mmoja ili kuokoa maisha ya ndugu zetu wanaopata huduma,” alisema Lulu.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo, Dkt. Msafiri Marijani alisema kwa niaba ya uongozi wa hospitali hiyo na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ya Zanzibar, wanaishukuru NSSF kwa kutoa vifaa tiba hivyo ambavyo vimetolewa kipindi ambacho hospitali hiyo ina uhitaji wa vifaa tiba mbalimbali na kuahidi vifaa hivyo kutumika kwa lengo lililokusudiwa.
Mwenyekiti wa Wanawake NSSF, Vaileth Segeja, alisema wametoa msaada huo kwa sababu Mfuko una sera ya kutoa misaada katika jamii, na kutoa wito kwa wanawake wote waliopo katika sekta isiyo rasmi kujiunga na Mifuko ya hifadhi ya jamii ukiwemo wa NSSF na ZSSF kwa ajili ya maisha yao ya sasa na baadaye.
Kwa
upande wake, Nassor Hassan ambaye ni Afisa Utawala wa ZSSF alisema kazi
kubwa ya Mifuko ya hifadhi ya jamii ni kuihifadhi jamii pale inapopata
janga ikiwemo ugonjwa na ndio maana NSSF iliamua kutoa msaada wa vifaa
tiba hivyo ili vikasaidie kuokoa maisha ya wananchi.
No comments:
Post a Comment