Shirika la Bima la Taifa (NIC)
limelipa shilingi milioni 46 kwa Kampuni 11 ambayo hununua mazao ya
korosho Mkoani Lindi na Mtwara na ambayo yamekata Bima kutoka NIC
kutokana na uharibifu wa mazao hayo.
Akizungumza na waandishi wa
mara baada ya kukabidhi hundi kwa wafanyabiashara wa Korosho Mkurugenzi
wa Masoko na Huduma kwa Wateja Yesaya Mwakifulefule amesema malipo ya
Bima hizo ni kutokana na hasara iliyotokana na unyaufu wa mzigo
koroshokuwa uliokua umehifadhiwa ktk maghala mbali mbali mikoani humo.
Mwakifulefule
amesema kuwa NIC iko katika kuhakikisha wafanyabiashara na wakulima
kupitia Bima ya Kilimo wanakuwa na na amani na uhakika wa mitaji yao
pindi wanapofikwa na majanga na kufanya biashara iendelee kutokana na
bima walizozikata kutoka NIC.
"Sisi ndiyo Bima tupo kwa ajili
kutoa huduma bora kwa wateja pamoja na kufanya biashara kuwa endelevu na
mitaji ikiwa salama kuendeleza kuwekeza maradufu katika sekta ya
kilimo"amesema Mwakifulefule.
Nae Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi Ghalani Sangye Bangu amesema kuwa
taasisi zingine ziige kwa bima pamoja na kutoa huduma.
Amesema kuwa wafanyabiashara katika sekta ya korosho wananeemeka na NIC kwa kwa kurudishiwa hasara waliopata uchakavu.
Mkurugenzi
wa Masoko na Huduma wa Shirika la Taifa la Bima (NIC) Yesaya
Mwakifulefule akizungumza mara baada ya kukabidhi hundi za Kampuni 11
zinazonunua Korosho katika Mikoa ya Lindi na Mtwara baada ya korosho
hizo kunyauka ,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Masoko na Huduma kwa Mteja Yesaya Mwakifulefule na Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi Ghalan Sangye Bangu
wakimukabidhi moja ya kampuni hundi mmoja wa kampuni zilizonunua
Korosho baada hapo zikanyauka ambapo Bima inalipa kutokana na unyaufu
huo jijino Dar es Salaam.
Mfanyabiashara wa Kampuni ya Amargo ,Amani Lila akizungumza baada ya kupata hundi kutoka NIC ,jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wafanyabiashara wa kanpuni za kununua korosho Lindi na Mtwara
wakisiliza mawasilisho ya watendaji wa NIC na Bodi ya Usimamizi wa
Stakabadhi Ghalani.jijini Dar es Salaam.
Post Top Ad
Your Ad Spot
Friday, March 11, 2022
NIC yalipa kampuni 11 zilizonunua korosho
Tags
BIASHARA#
Share This
About kilole mzee
BIASHARA
Labels:
BIASHARA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Your Ad Spot
No comments:
Post a Comment