A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, October 17, 2021

SIMBA YAIKANYA GALAXY NYUMBANI KWAO,

 

245841136_2666186247016353_4843876855356425977_n

Mwandishi wetu | MABINGWA watetezi wa ligi kuu Tanzania bara Simba leo wameibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Jwaneng Galaxy katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya kwanza uliopigwa Botswana.

Simba ilianza kupata bao la kwanza dakika ya pili ya mchezo kupitia kwa kiungo wake Taddeo Lwanga aliyepiga shuti kali baada ya mpira wa kona uliopigwa na Rally Bwalya na kimalizia na John Bocco .

Katika dakika ya 6 simba ilifanikiwa kuongoza bao la pili lililofungwa na nahodha wa timu hiyo John Bocco.
245925976_1292050531255940_6594856051076813004_n
Baada ya mabao hayo mawili ya mapema, Galaxy walianza kutafuta mabao ya kusawazisha lakini walijikuta wakikwama kwenye ukuta wa Simba uliokuwa unalindwa mabeki'.

Matokeo hayo yanakuwa na faida kubwa kwa Simba kwani Jwaneng watakuwa na kibarua kizito cha kupindua matokeo wakati watakapokuja kwenye mchezo wa marudiano utakaofanyika Octoba 24, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
246083604_1021801848670611_546552620653757577_n

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages