Na Alloyce Muta-Dar
Wasanii
mahiri wa kike ambao pia wamekuwa katika ushindani kimuziki Rubi na
Nandy leo wataonesha kuwa wanawake wakiwa na lao wanaungana.
Tamasha
hilo linaloenzi nia ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza
Michezo ni la kwanza hapa nchini kwa wanawake kucheza michezo wao
wenyewe.
Baada ya miaka mingi ya kukwepana na kila mmoja
kuonekana anapania kufanya vizuri zaidi ya mwenzake leo Jumamosi,
Septemba 18, 2021, Tamasha la Michezo ya Wanawake la Tanzanite
linawakutanisha kwenye Uwanja wa Uhuru hapa Dar es Salaam.
Michezo
mingi leo ikiwa ni siku ya tatu tayari imeanza asubuhi na itaendelea
hadi jioni ambapo saa kumi jioni Simba Queen itaoneshana ubabe na Timu
ya Taifa ya Wanawake U23 kwenye Uwanja huo wa Uhuru.
“Wasanii
zaidi ya 10 watakaopanda stejini leo wakiwemo Nandy na Rubi watu
wajazane uwanjani kabla ya saa nane kwani baada ya hapo kutakuwa na
ufunguzi na wasanii hawa watatumbuiza mpaka jioni,” ametangaza MC wa
sherehe hizo jana jioni wakati wa mapambano ya ndodi uwanjani hapo.
Wasanii
wengine wakali wa kike wanaotarajiwa kuwepo leo (wakisindikizwa na kaka
yao mkali wa Singeli Sholo Mwamba) ni Angela wa Konde Gang, Linnah,
Lulu Diva, Malkia Hadija Kopa, Shilole, mkali wa hip hop Rosaree na
wengine wengi.
No comments:
Post a Comment