Mkurugenzi
wa Fahari Tuamke Maendeleo Neema Mchau akiongea na Wazazi wa
Gongolamboto katika mahafali ya 17 Shule ya Msingi Ulongoni jana.
NA: HERI SHAABAN (ILALA )
MKURUGENZI
wa Fahari Tuamke Maendeleo Neema Mchau amewataka wazazi kusingatia
Elimu katika kufatilia Maendeleo ya watoto wao wasome mpaka kufikia vyuo
Vikuu ili Serikali iweze kupata viongozi bora.
Neema
Mchau aliyasema hayo katika mahafali ya 17 Shule ya Msingi Ulongoni
ambapo alikuwa mgeni rasmi katika shule hiyo ambapo katika hotuba yake
Neema aliwaasa Wazazi kuzingatia elimu kwa kuwaendeleza watoto waweze
kusoma kumaliza darasa la saba sio mwisho wa Elimu kwani elimu aina
mwisho watoto wana haki ya kupata elimu bora.
"Taifa
lolote ili liweze kuendelea Wananchi wake lazima wapatiwe elimu bora
sio bora Elimu nawaomba wazazi na jamii kwa ujumla marufuku tusiwapeleke
watoto kwa ndugu baada kumaliza elimu ya Msingi kwani bado watoto wana
haki ya kuendelea na elimu ya sekondari mpaka vyuo kumaliza elimu ya
Msingi sio mwisho wa Elimu" alisema Neema Mchau
Neema
alisema Dunia imeharibika katika kipindi cha Utandawazi kila mzazi ana
jukumu la kulea mtoto wake mwenyewe kwa Usalama wa Watoto wetu sio
busara kumpa MTU mtoto wako akulelehe .
Neema
aliwataka wazazi kuzingatia elimu na kuunga mkono juhudi za Serikali za
elimu bila malipo katika kuwasimamia watoto waweze kusoma na kuwa
viongozi wa baade.
Alisema
katika sekta ya elimu inawaibua wataalam wengi wakiwemo wataalam,
Madaktari, Mawaziri ,Waandisi, Wabunge ,Mawaziri kutokana na msingi bora
wa elimu ambao jamii watawekea vizazi vyao.
Aidha
Neema Mchau ambaye ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo
alichangia viti 20 kwa ajili ya Walimu wa shule hiyo ya Msingi Ulongoni
Wilaya ILALA.
Taasi ya Fahari Tuamke Maendeleo inamiliki Shule ya watoto Day Care Gongolamboto Wilaya ILALA .
No comments:
Post a Comment