A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, August 31, 2021

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA BUNGE LEO AGOSTI 31,2021 JIJINI DODOMA

 

Spika wa Bunge, Job Ndugai akiingia Bungeni kuongoza Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge, Job Ndugai akiongoza Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Bungeni 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Selemani Jafo (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Uwekezaji, Mhe. Geoffrey Mwambe wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Bungeni Jijini Dodoma,

Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Mhe. Emmanuel Mwakasaka akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Jijini Dodoma, 


Waheshimiwa Wabunge wakisimama kumkumbuka aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Hayati Elias Kwandikwa wakati wa kikao cha kwanza cha Mkutano wa Nne wa Bunge la 12 Bungeni Jijini Dodoma.


Waheshimiwa Wabunge wakishiriki kikao cha kwanza cha Mkutano wa Nne wa Bunge la 12 Bungeni Jijini Dodoma.




Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deo Ndejembi akijibu hoja za Waheshimiwa Wabunge wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Bungeni Jijini Dodoma,


Wanakwaya wa ofisi ya Bunge wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 12 Mkutano wa Nne Kikao cha Kwanza Bungeni Jijini Dodoma, Agosti 31, 2021

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages