A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, July 9, 2021

NDC KUSAIDIA WAKULIMA KUSAFIRISHA BIDHAA ZAO

Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo akizindua tela maalumu kwaajili ya kubebea mazao na bidhaa mbali mbali za wakulima. Uzinduzi huo umefanyika katika banda la NDC katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo akizungumza na waandishi wa habari katika Uzinduzi wa tela maalumu kwaajili ya kubebea mazao kwa mkulima. Uzinduzi umefanyika katika banda la NDC katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yabayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara  Exaud Kigahe (wa kwanza kulia), Mkurugezi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Edwin Rutageruka (wa kwanza kushoto),  na Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa NDC, Rhobi Sattima baada ya kuzindua tela maalumu kwaajili ya kubebea mazao ya mkulima.Uzinduzi umefanyika katika banda la NDC katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yabayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi  Mwendeshaji wa Shirika la Taifa la maendeleo  (NDC), Rhobi Sattima akizungumza na waandishi wa habari katika Uzinduzi wa tela maalumu kwaajili ya kubebea mazao kwa mkulima. Uzinduzi huo mefanyika katika banda la NDC katika Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yabayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo amelipongeza Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kwa kushirikiana na TEMDO pamoja na CARMATEC kwa kutengeneza Tela litakalosaidia wakulima wakulima kusafirisha mazao na pembejeo katika sekta ya kilimo.

 Tela hilo limetengenezwa na kiwanda cha KMTC ambacho husimamiwa na NDC.

Profesa Mkumbo ameyasema hao leo Julia 7,2021 wakati akizindua Tela hilo katika Maonesho ya 45 ya biashara ya Kimataifa ya yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere  Jijini Dar es Salaam.

Amesema  Mazao mengi ya wakulima yamekuwa yakiaribika njiani kabla ya kufika sokoni kutokana na changamoto ya usafiri hivyo Tela hilo linaenda kuwa tiba bora kwa wakulima na litawapunguzia gharama za kusafirisha mizigo na bidhaa.

"Tela hili limetengenezwa hapa hapa Tanzania , ambapo  kiwanda chetu cha KMTC kipo, hii inaonesha kwamba viwanda vyetu kwakweli vinaweza kutengeneza bidhaa za msingi  na moja ya malengo yetu ni kukidhi mahitaji ya soko la ndani ili tuanze kutumia na kula bidhaa ambazo tunazalisha sisi wenyewe hapa". Amesema Prof.Mkumbo.

Nae Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.Exaud Kigahe amesema uzinduzi wa tela hilo utaenda kuongeza thamani ya uzalishaji hasa katika sekta ya kilimo ambapo moja wapo ya changamoto kubwa ni kwenye usafirishaji mazao na bidhaa mbalimbali.

" Bidhaa zinakuwa zinaharibika au kutokufika kwa urahisi katika maeneo husika kwasababu ya kukosa vifaa maalumu na vya bei rahisi kwaajili ya kusafirishia mazao hayo na bidhaa mbalimbali". Amesema Mhe.Kigahe.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Taifa la maendeleo  (NDC), Bi.Rhobi Sattima amesema kuwa tela hilo lenye uwezo wa kubeba tani tano limebuniwa kwa kuzingatia vigezo vyote vya ubora, ufanisi na usalama wakati linapokuwa linafanya kazi na kuthibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Amesema kuwa tela hilo limetokana na wazo bunifu la kuwa na chombo cha kusafirisha pembejeo na mazao ya kilimo  ambalo litakokotwa na trekta linalounganishwa katika kiwanda cha matrekta  kilichopo katika eneo la mitaa ya Viwanda  TAMCO, Kibaha.

"Tela hili limesafiniwa kwa ushirikiano kati ya  NDC,TEMDO na CARMATEC. NDC walitoa wazo bunifu, TEMDO walihusika katika usanifu na michoro na CARMATEC walihusika katika  kufanya majaribio ya tela hili". Amesema Bi.Sattima.

Amesema moja ya mchango wa tela hilo kwenye uchumi ni  pamoja na mapinduzi kwenye sekta ya kilimo kwani mkulima  anaweza kuzalisha bila ya kuwa na changamoto ya usafirishaji wa mazao na pembejeo.

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages