A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, May 5, 2021

CCM YASEMA WAPINZANI KUSHINDWA NI LAZIMA MAJIMBO YA BUHIGWE, MUHAMBWE

 


Na Mwandishi  Wetu, Kigoma 

KATIBU  wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi( CCM) Shaka Hamdu Shaka ameufananisha uchaguzi  mdogo wa majimbo ya Muhambwe na Buhigwe kama vita vya Kagera  vilivyomgaragaza na kumuondoa Nduli Idd Amin  Dada na majeshi yake ndani ya  mipaka ya Tanzania mwaka 1978/1979 .

Amesema ni lazima adui apigwe bila huruma na kuhakikisha majeshi yao yanafukuzwa hadi nje ya karibu na mipaka  ya DR Congo. 

Shaka ameeleza hayo alipokuwa akitumia lugha ya kifasihi katika  uzinduzi  wa mkutano  wa hadhara wa kampeni huko Kibondo mkoani  Kigoma hapa mbele ya mgeni  rasmi Mjumbe wa kamati kuu ya  CCM Majaliwa Kasim Majaliwa.

Amesema mwaka 1978 nchi yetu ilivamiwa na majeshi ya Uganda tukalazimika kuyachakaza. Kipigo kama kile kitawapata tena watani  wao  Muhambwe na Buhingwe.

Amesema sababu ya watani kupigwa watani zipi nia na uwezo  wa kuwatandika upo hivyo kazi  iliobaki ni moja tu ya kuwashinda kwenye chaguzi zote mbili   kwenye majimbo hayo.

" Chama kimeweka dago Muhambwe na Buhigwe kuhakikisha tunashinda kwa haki, amani na kwa ushindani  wa kidemokrasia  .CCM ni waumini wa demokrasia shirikishi . Tumeshaingia kwenye  uwanja wa mapambano hatutarudi nyuma hadi ushindi utakapopatikana,, "amesisitiza  Shaka 

Ameongeza katika uchaguzi huo watashinda kwa mbinu za matumizi ya  sera na sayansi ya siasa hatimaye kuwaacha mbali  washindani wao kwani baadhi ya vyama vinashiriki  uchaguzi huu kwa lengo la kusindikiza  Chama Cha Mapinduzi na wagombea wake.

"Tumebeba baadhi ya mitambo  muhimu inayoweza kupiga  katika masafa mafupi na marefu .Kazi ilio mbele yetu ni kuwatandika bila huruma watani wetu ili kuwafundisha nidhamu ya siasa ,maana ya uchaguzi na CCM kilivyo makini" amesema.

Aidha amesema kwamba kwa Katiba ya Chama hicho wamefanya vikao vyake kuanzia ngazi za chini hadi  juu vya  kuyapitisha majina ya wagombea walioingia kuwa  sifa na walioshiriki kwenye  mchakato huo wanaendelea kutoa ushirikiano kwa wenzao. 

"CCM si chama cha nongwa au mizengwe au kuwekeana mifundo na vinyongo. Uchaguzi ndani ya chama unapomalizika kila mwanachama hutakiwa kuheshimu maamuzi. Jeshi letu ni moja hivyo kila askari hutakiwa kwenda mstari  wa mbele,"amesema Shaka. 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages