A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, April 27, 2021

Yanga yaifuata Tanzania Prisons

 


Kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nassreddine Nabi leo Aprili 27 kimekwea pipa kuwafuata wapinzani wao Tanzania Prisons, Rukwa,Songea.

Yanga ina kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali na ikiwa itashinda inatinga hatua ya nusu fainali ikipoteza itakuwa haina nafasi ya kusonga mbele. 

Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Aprili 30, Uwanja wa Nelson Mandela na mabingwa watetezi wa taji hilo ni watani zao wa jadi Simba.

Nahodha Msaidizi wa Yanga, Haruna Niyonzima amesema kuwa wana nafasi ya kupata ushindi kwenye mechi ambazo zimebaki na watapambana kufanya vizuri.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages