A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, April 30, 2021

Ecobank Tanzania Yatoa Elimu Kwa Wabunge Kuhusu Huduma Za Kibenki

 Kitengo cha Wateja Binafsi cha Ecobank Tanzania kikiongozwa na Mkuu wa kitengo cha wateja binafsi, Salma Mkambara imetembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutoa elimu kwa Waheshimwa wabunge na wafanyakazi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu huduma za Kibanki zinazotolewa na Benki hiyo.

Ecobank Tanzania inaendelea kuunga mkono mikakati ya Serikali ya kuongeza tija katika sekta ya huduma za fedha na kupanua huduma hizo ili kuwafikia watanzania walio wengi na ambao hawajafikiwa na huduma za kibenki.

Mkuu wa kitengo cha Wateja binafsi kutoka Ecobank Tanzania, Salma Mkambara pamoja na Meneja Mahusiano wa wateja Maalum kutoka Ecobank Tanzania Jackline Nyangoe wakimsikiliza Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai aliokuwa anauliza maswali kuhusu huduma zitolewazo na Benki hiyo wakati wa kutoa elimu kwa wabunge na wafanyakazi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai akisoma moja ya vipeperushi vya Ecobank Tanzania alipotembelea banda la benki hiyo kwa ajili yakupata elimu kuhusu huduma za Kibanki zinazotolewa na Benki hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo.
Mkuu wa kitengo cha Wateja binafsi kutoka Ecobank Tanzania, Salma Mkambara(kushoto) akizungumza na Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai(wa pili kushoto) pamoja na mbunge mwingine kuhusu namna Benko hiyo ilivyojipanga kuwafikia watu wengi hapa nchini wakiwemo wabunge. Wa pili kulia ni Meneja Mahusiano wa wateja Maalum kutoka Ecobank Tanzania Jackline Nyangoe
Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai akiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa wa Ecobank Tanzania mara baada kupata elimu kuhusu huduma za Kibanki zinazotolewa na Benki hiyo Bungeni Jijini Dodoma leo.

 Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi(kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Mahusiano wa wateja Maalum kutoka Ecobank Tanzania Jackline Nyangoe mara baada ya kutembelea Banda la benki hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages