A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Friday, August 21, 2020

Manispaa Ya Ilala: Hakuna Kumsajili Mfanyabiasha Wa Kemikali Bila Kibali Cha GCLA

 Na Chalila Kibuda,Michuzi TV


Manispaa ya Ilala imesema kuwa maafisa biashara katika Manispaa hiyo kuhakikisha hawaruhusu watu kufanya biashara ya kemikali, bila kuwa na kibali kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa serikali (GCLA).

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Ilala Jumanne Shauri  wakati akifunga mafunzo kwa Maafisa Biashara wa Manispaa hiyo ,jijini Dar es Salaam.

Amesema Kemikali kuwa wafanyabiashara wanaohitaji leseni wanatakiwa kuwa na kibali cha GCLA.

Shauri amesema mafunzo hayo ni  mafunzo maalum kwa maafisa biashara kuwa uwezo kudhibiti kemikali zinazoingia katika njia zisizo sahihi na kuleta madhara kwa wananchi na kusababisha serikali kutumia fedha nyingi kutatua tatizo la kemikali.

Amesema zipo  aina mbalimbali za dawa ambazo zimepigwa marufuku kutokana na athari zake kwa wananchi hivyo watu wakipata leseni lazima wafuatiliwe zaidi kwa kushirikiana na GCLA.

"Msipopata kibali kutoka GCLA  kuhusiana na kemikali  kutumika,  ni vyema maafisa  biashara msitoe leseni “amesema Shauri

Shauri  aliwataka  maafisa hao kuhakikisha leseni wanazotoa kwa wafanyabiashara, ziwe  na lengo la  kulinda afya ya walaji na mazingira  kwa mustakabali wa kizazi cha sasa na cha baadae.

Akizungumza katika mafunzo hayo Mkemia Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya (DCEA) Ziliwa Machibya alisema, umakini mkubwa unahitajika katika kudhibiti kemikali kwani nchi nyingi zimepata matatizo ya kemikali kutokana na kukosa udhibiti

“Wafanyabiashara kwa wakati mwingine, hutumia kemikali ambazo hazijadhibitiwa kutengeneza dawa za kulevya au kemikali zilizopigwa marufuku.

“Potassium permanganate  inatumika kusafishia maji lakini ikitumika vibaya watu hutengenezea Kokeini  hivyo kemikali hizi bashirifu (zilizoruhusiwa) kutokana na kwamba haziepukiki lazima  kudhibiti ili kuepusha uchepushaji”alisema.

Machibya alisema miongoni mwa changamoto zilizopo sasa katika udhibiti wa kemikali,  ni kuongezeka kwa wataalam katika maabara za siri  na usiri katika maabara juu ya utengenezaji wa kemikali hizo,

Meneja wa Kanda ya Mashariki Dunstan Mkapa wa GCLA  amesema mafunzo hayo ni kutaka maafisa biashara kuwa na ukaribu na GCLA wakati wanatoa leseni kuwa na kibali kutoka katika mamlaka hiyo.

Kwa upande wake Mkaguzi wa kemikali GCLA Emanuel Lewanga alisema katikka kudhibiti athari za kemikali katika jamii kampuni ndani za halmashauri zinazohusika kukusanya kemikali taka kwaajili ya uteketezaji wanapaswa kujisajili.

Hiyo ni  kwa mujibu wa sheria ya  usimamizi  wa matumizi ya kemikali majumbani na viwandani namba 3  ya mwaka 2013  sura ya 182 .

“Tumewaelekeza maafisa biashara ambao ndio watu wa msingi sana  kwamba  mtu anayetaka kujishughulisha na biashara ya  kemikali  lazima asajiliwe GCLA ikiwemo na  wale wanaokusanya taka zitokanazo na kemikali”alisema.

Amesema athari ambazo zinaweza kutokea endapo mtu hakusajiliwa kujihusisha na masuala ya kemikali, ni uteketezaji unaoweza kuleta athari kwa wananchi.
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Jumanne Shauri akizungumza wakati wa kufunga mafunzo kwa maafisa biashara wa manispaa hiyo kuhusiana na utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara wa Kemikali iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA)
 Mkaguzi wa Kemikali wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Emanuel Lewanga akitoa mada ya kemikali kwa maafisa biashara wa Manispaa ya Ilala katika mafunzo yaliyoandaliwa na GCLA jijini Dar es Salaam.
 Mkemia Mwandamizi wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya (DCEA) Kiliwa Machibya akitoa mada ya Kemikali Bashirifu katika mafunzo ya maafisa biashara wa Manispaa ya Ilala.
 Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) Dunstan Mkapa akitoa maelezo kuhusiana na mkakati wa utoaji wa mafunzo ya Kemikali kwa maafisa biashara.
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Jumanne Shauri akiwa katika picha ya pamoja na maafisa biashara wa manispaa hiyo na Watendaji wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia mkuu wa serikali GCLA mara baada ya kufunga mafunzo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages