A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, July 30, 2020

Kamishna Wa Tume Ya Uchaguzi NEC Jaji Mery Langwai Ataka Maafisa Uchaguzi Kutoa Elimu Ya Uchaguzi Kwa Watendaji Ngazi Ya Kata

Na Amiri Kilagalila,Njombe
Tume ya taifa ya uchaguzi NEC imehitimisha mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo watumishi 126 kutoka mikoa mitatu ya nyanda za juu kusini mwa Tanzania watakaohusika katika mchakato mzima wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika octoba 28 mwaka huu.
Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yalitolewa kwa waratibu wa uchaguzi wa mikoa ,wasimamizi wa uchaguzi,maafisa uchaguzi na Ugavi kutoka mikoa ya Njombe,Ruvuma na Iringa kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi jaji Mery Langwai amesema uwezo waliojengewa ukatumike ipasavyo katika kutekeleza majuku yao bila kuvunja sheria ,taratibu na kanuni za uchaguzi.
“Nina amini mafanikio katika mafunzo haya yanabashiri uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza katika mafunzo kwa watendaji ngazi ya kata na vitu vya kupiga kura kadri hatua yautekezaji wa uchaguzi kwa namna nzuri na uelewa mpana”alisema Jaji Merry Langwai
Katika hatua nyingine Jaji Langwai ameagiza watumishi hao kwenda kuipeleka elimu hiyo kwa wasimamizi wa uchaguzi wa uchaguzi ngazi ya kata na vituo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi katika kipindi chote cha uchaguzi.
“Jukumu lililo mbele yenu ni kutoa mafunzo kwa wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya kata na baadaye mtatoa mafunzo kwa makarani waongozaji,wasimamizi na wasimamizi wasaidizi kutoka katika halmashaui zenu”aliongeza Merry Langwai
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Iddy Mponda,Lucy Komba na Hamad Njovu wanasema mafunzo hayo yametolewa katika muda muafaka na kuahidi kwenda kusimamia zoezi la uchaguzi kwa umakini na kuzingatia misingi na taratibu ili kupata viongozi bora wa kuwatumikia watanzania katika kipindi kingine cha miaka 5.
“Mafunzo tuliyoyapata kwanza yametujengea uelewa wa kutosha hususani kwenye sharia yenyewe ya uchaguzi lakini pia taratibu zinazotkiwa kufuatwa kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa huru na haki”alisema Iddy Mponda.
 Baadhi ya washiriki wa semina Uchaguzi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri yam ji wa Njombe
  Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi jaji Mery Langwai wakati akitoa hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu kwa wasimamizi wa Uchaguzi katika ukumbi wa halmashauri yam ji wa Njombe Lunyanywi.
 Baadhi ya washiriki wa semina ya uchaguzi kutoka NEC wakimsikiliza kamishna wa tume ya taifa ya Uchaguzi wakati akifunga mafunzo ya siku tatu mjini Njombe

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages