A great place to access the latest news and information.

Breaking

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, July 15, 2020

BENKI YA NMB YATOA MSAADA WA MILIONI 36 KWA SHULE ZA SEKONDARI TANGA

Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB, Benedicto Baragomwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakiwa wameshika madawati yaliyokabidhiwa na benki ya NMB kwa ajili ya shule saba za jijini Tanga kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Sekondari ya Pongwe nje kidogo ya Jiji la Tanga. Kutoka kushoto ni Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Aikansia Muro, katikati mwenye miwani ni Meneja wa NMB Madaraka, Elizabeth Chawinga na mwisho kulia ni Mkurugenzi wa jiji la Tanga, David Mayeji.
Benki ya NMB imetoa msaada wenye thamani ya shilingi Milioni 36 kwa shule Saba za Sekondari; Kirare, Japan, Chongoleani, Nguvumali, Pongwe na Galanos za Jijini Tanga, kwa kuzipatia madawati 250 pamoja na mabati 352 ili kutatua changamoto za kielimu.

Akikabidhi msaada huo katika Shule ya Sekondari ya Pongwe kwa Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki hiyo, Benedicto Baragomwa alisema, wamekuwa mstari wa mbele kushiriki kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi.

Alisema kwa upande wa sekta ya elimu, kipaumbele wamekiweka kwenye madawati, vifaa vya kuezekea huku kwenye afya wakitoa vifaa vya tiba kama vitanda vya kujifungulia wakina mama na vitanda vya wagonjwa na magodoro yake vilevile na kusaidia majanga yanayoipata nchi.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages